-
Je, Utatembea Pamoja na Mungu?Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
-
-
5. Kwa nini Yesu alizungumza kuhusu kuongeza kipimo cha mkono mmoja kwenye uhai wa mtu?
5 Mara nyingi Biblia hufananisha maisha na safari au kutembea. Katika visa fulani, ulinganifu huo huonyeshwa kwa njia ya moja kwa moja, lakini katika visa vingine, huonyeshwa kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Kwa mfano, Yesu alisema: “Ni nani kati yenu kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mkono mmoja kwenye uhai wake?” (Mathayo 6:27) Huenda ukashangazwa na jambo fulani kuhusu maneno hayo. Kwa nini Yesu alitumia kipimo cha umbali badala ya kipimo cha wakati alipozungumza kuhusu kuongeza “kipimo cha mkono mmoja” kwenye uhai?a Inaonekana Yesu alikuwa akilinganisha uhai na safari. Hivyo, alikuwa akifundisha kwamba kuhangaika hakuwezi kukusaidia kuongeza hata hatua ndogo katika safari yako ya maisha. Lakini, je, hiyo inamaanisha kwamba hakuna kitu tunachoweza kufanya kuhusiana na muda ambao tutatembea? Bila shaka la! Hilo linatuleta kwenye swali letu la pili, Kwa nini tunahitaji kutembea pamoja na Mungu?
-
-
Je, Utatembea Pamoja na Mungu?Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
-
-
a Tafsiri fulani za Biblia zimebadili “kipimo cha mkono mmoja” katika mstari huo kuwa kipimo cha wakati, kama vile, “muda” (Biblia Habari Njema) au “saa moja” (Neno—Agano Jipya). Hata hivyo, neno la awali lililotumiwa linamaanisha kihalisi kipimo cha mkono mmoja, ambacho kilikuwa na urefu wa sentimeta 45 hivi.
-