-
“Jitahidini”Mnara wa Mlinzi—1986 | Januari 15
-
-
2. (a) Kwa sababu gani wokovu hauwezi kuchumwa? (b) Maneno ya Yesu kwenye Luka 13:24 yanaonyeshaje jambo linalotakwa ili kupata wokovu?
2 Wokovu hauwezi kuchumwa kwa kuhudhuria mikutano wala kwa njia nyingineyo yote. Huo unapewa bure, ni zawadi kutoka kwa Mungu. Hata hivyo, Yehova Mungu anataka sisi tufanye jitihada fulani-fulani ndipo tuipokee zawadi yake ya uzima wa milele. (Warumi 6:23) Jitihada gani? Moja ni kujikaza kwa bidii nyingi katika utumishi wake! Ni lazima vitendo hivyo visukumwe na uthamini wa kweli. Wakati mmoja Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliulizwa hivi na mwanamume mmoja: “Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache?” Jibu la Yesu halikumhusu muulizaji peke yake bali pia wengine wote waliopendezwa kupata wokovu, kutia na sisi. Alijibu: “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.”—Luka 13:23, 24.
3. (a) Kwa sababu gani ulizo la mwanamume yule lilikuwa lisilo la kawaida? (b) Yesu anatuhusishaje katika jibu lake?
3 Ulizo la mwanamume huyo asiyetajwa jina lilikuwa lisilo la kawaida. Yeye aliuliza: “Watu wanaookolewa ni wachache?.” si “Je, mimi nitakuwa kati ya wachache watakaookolewa?” au “Mimi naweza kuokolewaje?” Labda kilichomfanya aulize ulizo lake la kutaka sana kujua ni ile falsafa ya Kiyahudi iliyosema kwamba ni hesabu ndogo tu ya watu wangestahili kupata wokovu.a Hata liwe ni jambo gani lililokuwa chanzo cha udadisi wake, Yesu alifanya haraka kuliondosha ulizo hilo kwenye kufikiria-fikiria tu na kulifanya lifaane na hali za kweli—liwe na matumizi ya kibinafsi. Alimlazimisha muulizaji afikirie alilohitaji kufanya ili apate wokovu. Lakini zaidi ya hilo, kwa kuwa maneno ya Yesu “jitahidini” yamesemwa kwa namna ya kuambia wingi wa watu, yanapasa yatuchochee tufikirie sana jinsi ibada yetu ilivyo.
-
-
“Jitahidini”Mnara wa Mlinzi—1986 | Januari 15
-
-
a Kati ya marabi, kulikuwa na ubishi mkubwa wa kidini juu ya hesabu ya wenye kuokolewa. Kitabu cha marejezo ya Biblia kinasema hivi: “Kati ya dhana za Kiyahudi ambazo Marabi walikuwa nazo, moja ilikuwa ni kujaribu kuweka hesabu ya wenye kuokolewa kwa kujumlisha tarakimu zilizosimamiwa na herufi za andiko hili na hili.”
-