Je! Wewe Unakumbuka?
Je! wewe umeyaona matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi yakiwa na thamani inayotumika kwako? Kwa nini basi usitahini kumbukumbu lako kwa mambo yanayofuata?
◻ Yesu alimaanisha nini aliposema kwamba hakuna mtu angeweza kuwa mwanafunzi wake asipochukia baba yake na mama na mke na watoto na ndugu na dada zake, ndiyo, hata nafsi yake mwenyewe’? Luka 14:26 NW)
Yesu hakumaanisha kwamba mmoja wa wafuasi wake anapaswa kuwachukia kihalisi watu wa ukoo wake au uhai wake mwenyewe. Bali, alimaanisha kwamba ni lazima mwanafunzi apende wengine au uhai wake mwenyewe kwa kadiri ndogo kuliko vile anavyompenda Yesu.—1/1, ukurasa 8.
◻ Ni mambo gani matatu ya msingi ambayo yamechangia fanikio la kazi ya kimisionari ya Mashahidi, wakati uliopita na wa sasa?
Moja ni kuwafikia watu kibinafsi kwenye nyumba zao. Jingine ni ule ujumbe wa Ufalme ulio wa moja kwa moja na rahisi ambao msingi wao ni Biblia. La tatu ni ule upendo kama wa Kristo unaodhihirishwa na wamisionari katika kushughulika na watu.—1/1, ukurasa 14.
◻ kwa nini kwa muda fulani Mungu aliongeza agano la Sheria kwenye agano la Kiabrahamu?
Agano la Sheria lilithibitisha kwamba Waisraeli walikuwa watenda dhambi wanaohitaji kuhani wa kudumu na dhabihu kamilifu. Lililinda ukoo wa yule Mbegu na kusaidia kumtambulisha Mbegu huyo. Pia lilionyesha kwamba siku moja Mungu angekuwa na taifa la wafalme-makuhani.—2/1,ukurasa 16.
◻ Ni nini maagano saba ya kimungu yanayofanyika hatua kwa hatua yakiongoza kwenye baraka za milele kwa ajili ya sisi sote?
Agano la Kiedeni, agano la Kiabrahamu, agano la Sheria, agano kwa ajili ya kuhani kama Melkizedeki, agano la Ufalme wa Kidaudi, agano jipya, na agano la Ufalme.—2/1, ukurasa 19.
◻ Je! yale maelfu ya mitofautiano iliyo katika hati-mkono za Biblia yanadhoofisha dai la Biblia kuwa ndilo Neno la Mungu?
Sivyo. Wanachuo wa Biblia wanatuambia kwamba karibu mitofautiano yote hiyo si ya maana kubwa kwenye andishi. Inasaidia tu kuimarisha uthibitisho wa ukweli wa Maandiko. (Zaburi 119:105; 1 Petro 1:25)—2/1, kurasa 29,30.
◻ Neno “mwagnosti” limetolewa kwenye nini, nalo linatumiwaje katika Biblia?
“Mwagnosti” limetolewa kwenye neno la Kigiriki aʹgno·stos, linalomaanisha ‘isiyojulikana.’ Paulo alitumia namna ya neno hilo katika hotuba yake kwa Waathene wakati aliporejezea madhabahu iliyowekwa wakfu ‘Kwa Mungu Asiyejulikana.’ (Matendo 17:23)—2/15, ukurasa 5.
◻ Inatupasa tutendeje wakati ambapo huenda mwelekezo fulani wa Kimaandiko ukaonekana kuwa unaweza kufanyiwa maoni tofauti-tofauti?
Inatupasa tuonyeshe itikio la unyenyekevu lililoonyeshwa na Wakristo wa mapema, tukikubali maamuzi na mielekezo kutoka kundi la Mungu. (Matendo 15:6-29)—2/15, ukurasa 20.
◻ Yesu alimaanisha nini aliposema: “Jifanyieni rafiki kwa mali ya udhalimu, ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele”? (Luka 16:9)
Inatupasa tuwe na bidii-endelevu ya kutumia utajiri wowote tulio nao ili kuunga mkono masilahi ya UfaIme na hivyo tusitawishe urafiki pamoja na Yehova na Mwana wake. Hao peke yao ndio wanaoweza kutuandalia mahali mbinguni au katika dunia-paradiso wakati mali za kimwili zinaposhindwa au kutoweka.—3/1, ukurasa 9.
◻ Ni mambo gani matatu yanayotakwa kwa upande wetu ili tunufaike kutokana na muono-ndani ambao Yehova anafanya upatikane?
Tunahitaji kuthamini tengenezo la Yehova; ni lazima tujifunze Neno la Mungu kwa ukawaida na misaada inayoandaliwa ambayo hutuwezesha tulielewe; na ni lazima tutafakari mambo ambayo tumejifunza na jinsi ya kuyatumia katika maisha yetu ya kila siku.—3/15, ukurasa 14.
◻ kwa nini watu wa Israeli ya kale walitenda kwa ukosefu mbaya sana wa muono-ndani?
Wao hawakufikiri sana kwa uthamini juu ya mambo yote ambayo Yehova alikuwa amewafanyia. (Zaburi 106:7, 13)—3/15, ukurasa 17.
◻ Ni nini kinachowakilishwa na “majeshi ya kikosi cha askari wapanda-farasi” yanayonenwa kwenye Ufunuo 9:16, NW?
Farasi hawa wa ufananisho hawawakilishi mabaki yanayopungua ya wapakwa-mafuta tu bali pia “mkutano mkubwa” unaoongezeka na ulio na nguvu nyingi wa “kondoo wengine.” (Ufunuo 7:9; Yohana 10:16)—4/1, ukurasa 19.