Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Hakuwa Akisema Nao Bila Mfano”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • 13 Yesu alitaja mambo mengine yanayojulikana kuhusu barabara ‘inayotoka Yerusalemu kwenda Yeriko.’ Kulingana na mfano huo, kuhani ndiye aliyepita kwanza katika barabara hiyo kisha akafuatwa na Mlawi, ijapokuwa hakuna yeyote kati yao aliyesimama kumsaidia mtu aliyejeruhiwa. (Luka 10:31, 32) Makuhani walitumikia hekaluni huko Yerusalemu, nao walisaidiwa na Walawi. Makuhani na Walawi wengi walikaa Yeriko wakati ambapo hawakuwa wakifanya kazi hekaluni, kwa kuwa Yeriko lilikuwa umbali wa kilometa 23 tu kutoka Yerusalemu. Kwa hiyo, walipitia barabara hiyo. Pia, ona kwamba Yesu alisema msafiri huyo alikuwa “akishuka,” bali hakuwa akipanda, barabara ‘inayotoka Yerusalemu.’ Wasikilizaji wake walielewa jambo hilo. Yerusalemu lilikuwa juu kuliko Yeriko. Basi, safari ya “kutoka Yerusalemu” ilikuwa ya ‘kushuka.’b Ni wazi kwamba Yesu aliwafikiria wasikilizaji wake.

  • “Hakuwa Akisema Nao Bila Mfano”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • b Pia, Yesu alisema kwamba kuhani na Mlawi huyo walikuwa wakija “kutoka Yerusalemu,” hivyo, walikuwa wakitoka hekaluni. Kwa hiyo, hakuna yeyote angeweza kusingizia kwamba walimwepuka mtu huyo aliyekuwa katika hali mahututi kwa sababu hawakutaka kuwa najisi kwa muda wasiweze kutumikia hekaluni.—Mambo ya Walawi 21:1; Hesabu 19:16.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki