-
Watie Moyo Wanawake WakristoMnara wa Mlinzi (Funzo)—2020 | Septemba
-
-
Kama Yesu, tunaweza kuwaonyesha dada zetu waaminifu kwamba tunawajali sana (Tazama fungu la 6 hadi 9)e
6. Kulingana na Luka 10:38-42, Yesu aliwasaidia Martha na Maria jinsi gani?
6 Yesu alitumia wakati wake pamoja na dada zake wa kiroho, naye alikuwa rafiki wa kweli. Fikiria urafiki wake pamoja na Maria na Martha, ambao inaelekea walikuwa waseja. (Soma Luka 10:38-42.) Ni wazi kwamba kupitia maneno na matendo yake, Yesu aliwastarehesha. Maria alijihisi huru kuketi miguuni pake kama wanafunzi wengine.c Na Martha alipokwazika kwa sababu Maria hakuwa akimsaidia kutayarisha chakula, alikuwa huru kumweleza Yesu hisia zake. Katika kikusanyiko hicho kisicho rasmi, Yesu aliweza kuwasaidia kiroho wanawake hao. Na alionyesha kwamba aliwajali wanawake hao na ndugu yao Lazaro, kwa kuwatembelea kwa ukawaida. (Yoh. 12:1-3) Haishangazi kwamba Lazaro alipokuwa mgonjwa sana Maria na Martha walijua kwamba wangeweza kumwomba Yesu awasaidie.—Yoh. 11:3, 5.
-
-
Watie Moyo Wanawake WakristoMnara wa Mlinzi (Funzo)—2020 | Septemba
-
-
c Kitabu kimoja cha marejeo kinasema hivi: “Wanafunzi waliketi miguuni pa walimu wao. Walifanya hivyo walipokuwa wakijiandaa kuwa walimu. Hata hivyo, wanawake hawakuruhusiwa kuwa walimu. Hivyo, inaelekea wanaume wengi wa Kiyahudi wangeshangazwa kumwona Maria ameketi miguuni pa Yesu, na akiwa na hamu ya kujifunza kutoka kwa Yesu.”
-