-
Alikata “Kauli Moyoni Mwake”Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 1
-
-
MARIA aliketi bila kustarehe juu ya punda. Alikuwa amesafiri kwa muda mrefu. Mbele yake, Yosefu alikuwa akitembea akiwaelekeza Bethlehemu iliyo mbali sana. Kwa mara nyingine, Maria alihisi kitoto kikicheza ndani yake.
Biblia inasema kwamba wakati huo Maria alikuwa “karibu kuzaa.” (Luka 2:5) Wenzi hao walipopita shamba moja baada ya lingine, huenda wakulima fulani waliwatazama na kujiuliza kwa nini mwanamke aliye katika hali kama hiyo angeamua kusafiri. Ni nini kilichomfanya Maria asafiri mbali hivyo kutoka nyumbani kwao Nazareti?
-
-
Alikata “Kauli Moyoni Mwake”Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 1
-
-
Hata hivyo, Luka anaandika kwamba Yosefu alienda “kuandikishwa pamoja na Maria.” Pia anasema kwamba Yosefu ‘alikuwa amemwoa Maria kama ilivyoahidiwa.’ (Luka 2:4, 5) Yosefu alikuwa na uvutano mkubwa sana juu ya maamuzi ya Maria kwa kuwa sasa Maria alikuwa mke wake. Maria alimwona mume wake kuwa kichwa chake kuhusiana na mambo ya kiroho, na alikubali jukumu lake alilopewa na Mungu la kuwa msaidizi wake kwa kuunga mkono maamuzi yake.a Kwa hiyo, alishinda kipingamizi hicho cha imani yake kwa kutii.
-