-
“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”Igeni Imani Yao
-
-
5. Maneno ya Yesu yanayomhusianisha Abeli na “kuwekwa msingi wa ulimwengu” yanamaanisha nini? (Ona pia maelezo ya chini.)
5 Abeli alizaliwa mwanzoni mwa historia ya wanadamu. Baadaye, Yesu alimhusianisha Abeli na “kuwekwa msingi wa ulimwengu.” (Soma Luka 11:50, 51.) Inaonekana Yesu alimaanisha ulimwengu wa watu walio na tumaini la kukombolewa kutoka katika dhambi. Ingawa Abeli alikuwa mtu wa nne kuishi duniani, inaonekana ndiye mtu wa kwanza ambaye Mungu aliona kuwa anaweza kukombolewa.a Ni wazi kwamba Abeli hakulelewa kati ya watu wenye uvutano mzuri.
-
-
“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”Igeni Imani Yao
-
-
a Maneno “kuwekwa msingi wa ulimwengu” yanahusiana na wazo la kupanda mbegu, yakimaanisha kuzaana, hivyo yanamhusu mzao wa kwanza kabisa wa wanadamu. Basi, kwa nini Yesu alihusianisha Abeli na “kuwekwa msingi wa ulimwengu” na si Kaini, ambaye alikuwa wa kwanza kuzaliwa? Maamuzi na matendo ya Kaini yalionyesha uasi wa kimakusudi dhidi ya Yehova Mungu. Kama wazazi wake, inaonekana Kaini hana tumaini la kukombolewa na kufufuliwa.
-