-
“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”Mnara wa Mlinzi—2013 | Januari 1
-
-
Abeli alizaliwa mwanzoni mwa historia ya wanadamu. Baadaye, Yesu alimhusianisha Abeli na “kuwekwa msingi wa ulimwengu.” (Luka 11:50, 51) Inaonekana Yesu alimaanisha ulimwengu wa watu walio na tumaini la kukombolewa kutoka katika dhambi. Ingawa Abeli alikuwa mtu wa nne kuishi duniani, inaonekana ndiye mtu wa kwanza ambaye Mungu aliona kuwa anaweza kukombolewa.a Ni wazi kwamba Abeli hakulelewa kati ya watu wenye uvutano mzuri.
-
-
“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”Mnara wa Mlinzi—2013 | Januari 1
-
-
a Maneno “kuwekwa msingi wa ulimwengu” yanahusiana na wazo la kupanda mbegu, yakimaanisha kuzaa, hivyo yanahusiana na mzao wa kwanza kabisa wa wanadamu. Hata hivyo, kwa nini Yesu alihusianisha Abeli na “kuwekwa msingi wa ulimwengu” na si Kaini, ambaye alikuwa mwanadamu wa kwanza kuzaliwa? Maamuzi na matendo ya Kaini yalitokeza uasi wa kimakusudi dhidi ya Yehova Mungu. Kama tu wazazi wake, inawezekana kwamba Kaini hana tumaini la kukombolewa na kufufuliwa.
-