-
“Kweli Ni Nini?”Mnara wa Mlinzi—1995 | Julai 1
-
-
“Kweli Ni Nini?”
WATU hawa wawili walioketi wakikabiliana walitofautiana kabisa. Mmoja alikuwa mwanasiasa mwenye madharau, aliyetamani makuu, tajiri, aliye tayari kufanya jambo lolote ili kuendeleza kazi-maisha yake mwenyewe. Yule mwingine alikuwa mwalimu aliyekataa utajiri na umashuhuri naye alikuwa tayari kudhabihu uhai wake ili kuokoa uhai wa wengine. Kwa wazi, watu hawa wawili hawakuwa na maoni sawa! Katika jambo moja hasa, hawakusikilizana kabisa—lile suala la kweli.
Watu hawa walikuwa Pontio Pilato na Yesu Kristo. Yesu alikuwa amesimama mbele ya Pilato akiwa mhalifu mshutumiwa. Kwa nini? Yesu alieleza kwamba sababu ya hilo—kwa kweli, sababu yenyewe iliyomfanya aje duniani na kuanzisha huduma yake—ilikuwa kitu kimoja: kweli. “Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni,” akasema, “ili niishuhudie kweli.”—Yohana 18:37.
Jibu la Pilato lilikuwa swali kubwa sana: “Kweli ni nini?” (Yohana 18:38) Je, hakika alitaka jibu? Labda sivyo. Yesu alikuwa mtu ambaye angejibu swali lolote aliloulizwa kwa unyofu, lakini hakumjibu Pilato. Na Biblia yasema kwamba baada ya kuuliza swali lake, Pilato alitoka mara hiyo nje ya ukumbi wake wa wageni. Yaelekea gavana huyo wa Roma aliuliza swali lake kwa madharau ya kutoamini, kana kwamba kusema, “Kweli? Hiyo ni nini? Hakuna kitu kama hicho!”a
-
-
“Kweli Ni Nini?”Mnara wa Mlinzi—1995 | Julai 1
-
-
a Kulingana na msomi wa Biblia R. C. H. Lenski, “sauti [ya Pilato] ni ile ya mtu asiyejali wa kilimwengu ambaye kwa swali lake akusudia kusema kwamba kitu chochote cha asili ya kweli ya kidini ni kisio bure tu.”
-