Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/15 uku. 27
  • Je! Wewe Unakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yohana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kitabu Cha Biblia Namba 43—Yohana
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kesi Mbele ya Sanhedrini, Kisha Apelekwa kwa Pilato
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/15 uku. 27

Je! Wewe Unakumbuka?

Je! wewe umeyapata matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi kuwa yenye thamani yenye mafaa kwako? Kwa nini usitahini kumbukumbu yako kwa maswali yanayofuata?

◻ Ni nini jibu kwa tatizo la leo la mimba za utineja?

Ni lazima vijana wapewe mwongozo wa kiadili na wa kiroho. Biblia inaonyesha kwamba wazazi ndio wenye daraka la kufanya hivyo. (Waefeso 6:4)—4/15, ukurasa 4.

◻ Ni jambo gani linalofanya iwe vigumu kulea watoto kwa mafanikio?

Wazazi na watoto ni wasiokamilika na, kwa sababu hiyo, wanafanya makosa. (Warumi 5:12) Pia, watoto wanaokua wanavutwa sana na maelekeo mabaya ya jamii ya watu wa kisasa; jambo hilo linaathiri vibaya sana maadili yao na matazamio ya mbele kuhusu maisha, (2 Timotheo 3:1-5)—5/1, ukurasa 4.

◻ Ni nini tofauti kubwa nne za kutokeza kati ya Wakristo wa kweli na wale wa jina tu?

Wakristo wa kweli wanashika mwiko wa damu. (Matendo 15:28, 29, NW) Wao wanadumisha viwango vya juu vya kiadili. (1 Wakorintho 6:9, 10) Wakristo halisi wanabaki bila kuwamo katika siasa na yale mahitilafiano mengi ya kitaifa. (Yohana 17:16) Wale wanaofuata Yesu wanatumia kielelezo chake kuwa kiolezo cha mahusiano yao ya kinyumbani. (Waefeso 5:21-25)​—5/1, kurasa 17-19.

◻ Kwa nini Wayahudi waliita Yesu Msamaria? (Yohana 8:48)

Wayahudi waliwachukia Wasamaria. Kwa sababu hiyo, neno hilo lilitumiwa nao kuwa usemi wa madharau na suto dhidi ya Yesu.​—5/15, ukurasa 8.

◻ Ni nini ile “lugha yenye kutakata” inayonenwa habari zayo kwenye Sefania 3:9, NW?

Hii ndiyo lugha ya ukweli wa Kimaandiko inayowezesha watu wenye kuogopa Mungu wa mataifa na rangi za jamii zote za watu watumikie Yehova bega kwa bega.​—5/15, ukurasa 16.

◻ Ni mauhuru gani yanayotokana na kusitawisha uhusiano pamoja na Mungu?

Uhuru wa kutokuwa na hofu yenye kutumikisha kwa mwanadamu na kutokuwa na desturi zenye kulemea zisizo na maana au thamani halisi. (Mithali 29:25) Pia, uhuru wa kutokuwa na hofu juu ya kifo. (Mhubiri 9:5,10; Yohana 5:28, 29)​—6/1, kurasa 5-6.

◻ Yesu alimaanisha nini aliposema:“Usiku unakuja ambapo mtu yeyote hawezi kufanya kazi”? (Yohana 9:4, NW)

Yesu alikuwa hapa akirejeza kwenye wakati ambapo yeye angekuwa ndani ya kaburi na hangeweza tena kufanya kazi za kustaajabisha alizokuwa amefanya alipokuwa hai.​—6/1, ukurasa 8.

◻ Ubatizo katika maji unamaanisha nini?

Uzamisho kamili katika maji ni ufananisho unaofaa wa wakfu wa mtu kwa Mungu, ambapo mmoja anakuwa mhudumu aliyeagizwa rasmi. Anapokuwa chini ya maji, inakuwa sawa na jambo la kwamba yeye amefia mwendo wake wa zamani wa maisha, na anapotoka ndani ya maji, inaweza kusemwa anakuwa hai kwa mwendo mpya wa kujidhabihu katika utumishi wa Yehova. (Linganisha Warumi 6:2-4; 12:1; Wafilipi 3:16.)—6/15, ukurasa 29.

◻ Ni nini baadhi ya njia za kuonyesha ushukuru kwa Yehova?

Wakati ushukuru unapokuwa imara, tamaa yenye kushurutisha kutumikia Mungu inajazana katika moyo wenye uthamini. Njia moja ya tamaa hii ni kujihusisha katika huduma, labda katika utumishi wa painia. Nyingine ni kufanya ushirikiano katika ile programu ya ujenzi inayotukia sasa kuzunguka dunia.​—7/1, ukurasa 11.

◻ Kwa nini Yesu aliwapa 70 kati ya wanafunzi wake nguvu za kuponya wagonjwa alipowatuma nje katika kampeni ya kuhubiri katika Galilaya?

Wanafunzi hawa, kwa kufanya miujiza hiyo, walitayarishia Yesu njia ya kufanya kazi ya ufuatishaji. Miujiza waliyofanya ingefanya wengi wa wale wenye nyumba wawe na hamu nyingi ya kukutana na Yesu na kusikiliza ujumbe wake wa Ufalme.​—7/1, kurasa 16-17.

◻ Je! Yesu alikuwa akirejeza kwa Yuda wakati Yeye alipoambia Pilato hivi: “Yeye aliyenitia mikononi mwako yu na dhambi iliyo kubwa zaidi”?​—Yohana 19:11.

Inaonekana kama kwamba Yesu alikuwa akirejeza kwa wote wale waliokuwa na daraka la kulaumika kwa sababu ya kujaribiwa kwake mbele ya Pilato. Kwa uhakika hiyo ilitia ndani Yuda Iskariote, aliyesaliti Yesu. (Luka 22:2-6) Lakini Kayafa kuhani mkuu na viongozi wengine wa kidini walihusika pia katika kutokeza kukamatwa kwa Yesu. (Mathayo 26:59-65; 27:1, 2, 20-23) Inaelekea kwamba hawa wote wenye hatia walitiwa katika yale ambayo Yesu alisema kwenye Yohana 19:11.​—7/15, ukurasa 30.

◻ Ni hatari gani yenye kuleta kifo hasa inayohusiana na ibada ya mifano?

Mtunga zaburi alisema hivi juu ya Waisraeli: “Wakitumikia sanamu za wapagani, wao walijipata wenyewe wametegwa ndani ya kudhabihu wana na binti zao wenyewe kwa roho wabaya.” (Zaburi 106:36, 37, The Jerusalem Bible) Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanaonya juu ya hatari hiyo hiyo. (1 Wakorintho 10:19, 20) Ibada ya mifano ya namna yo yote inafungulia uwezekano wa kwamba mfano utatumika kama mahali pa kupashana habari na kani za roho wabaya.​—8/1, kurasa 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki