Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 4/15 uku. 31
  • Je! Unakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Wapanda Farasi wa Kitabu cha Ufunuo—Jinsi Unavyopatwa na Matokeo ya Upandaji Wao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kulifumbua Fumbo la Wapanda-Farasi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Wapanda Farasi Wanne​—Jinsi Wanavyokuhusu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 4/15 uku. 31

Je! Unakumbuka?

Je! umefikiria kwa makini matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, inaelekea kuwa utakumbuka mambo yanayofuata:

◻ Ni kwa kadiri gani Yesu aliwaonyesha wanadamu upendo?

Yeye aliyaacha makao ya kimbingu yenye amani na usalama kwa kujitolea mwenyewe ili aje ale, alale, na kushirikiana pamoja na wanadamu wenye kuugua-ugua na kufa. Baada ya hapo, Yesu aliyatoa maisha yake ya kuwa mwanadamu mkamilifu ili aandae ukombozi kwa faida ya wanadamu. (Mathayo 20:28) —12/15, kurasa 3, 4.

◻ Ni faida gani za kibinafsi zinazotokea kwa Mkristo anayesitawisha kujiweza?

Mkristo huyo anapata hali bora ya kujiheshimu kwa kujizoeza kujiweza. Pia, anafurahia amani na furaha kubwa zaidi katika uhusiano wa jamaa, wa kundi na wa kila siku. Juu ya yote, kujiweza kunamhakikishia kuwa na uhusiano mwema pamoja na Muumba wake, na kunasaidia kumtambulisha kuwa Mkristo wa kweli.—12/15, ukurasa 24 (Kiingereza).

◻ Kusudio la msingi la kuonyesha ukaribishaji linapasa kuwa nini?

Ingawa inaridhisha kuambiwa na wengine maneno ya shukrani na kutambua kwamba jitihada zetu zimethaminiwa, imetupasa tutake kuonyesha ukaribishaji hasa kwa sababu hilo ndilo jambo linalofaa na la upendo kufanya. Zaidi ya hilo, Yehova Mungu anafurahi tukifanya hivyo.—1/15, ukurasa 22 (Kiingereza).

◻ Mpandaji aliye juu ya yule farasi mweupe, anayeelezwa katika Ufunuo 6:2, ana matokeo gani juu ya maisha yako?

Yesu ndiye mpandaji aliye juu ya yule farasi mweupe, naye alianza upandaji wake wa kimbingu mwaka 1914. Akitabiri jinsi watu wangehusiwa na utawala wake alisema: “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake . . . atawabagua [watu] kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi.” Leo, wanadamu wote wanaendelea kubaguliwa, na njia yako ya kuuitikia ujumbe wa Ufalme itamaanisha ama uzima ama kifo kwako. (Mathayo 25:31-33; 24:14) — 1/15, ukurasa 6.

◻ Ni baadhi ya njia zipi anazotumia Yehova kufariji na kutegemeza watumishi wake?

Yehova anafariji na kutegemeza watumishi wake kupitia roho takatifu yake. (1 Petro 4:12-14) Anawafariji pia kwa kujibu sala zao. (Wafilipi 4:6, 7) Tena, Neno la Mungu ni chanzo kikubwa cha faraja, kinachohakikishia watumishi wake kwamba hakuna jambo linaloweza kuwapata ambalo Yehova haoni wala hawezi kuzuia.—2/1, ukurasa 19 (Kiingereza).

◻ Ni nini Ufunuo unaotabiriwa katika Biblia?

Ni hatua ya Mungu ya kuingilia mambo ya kibinadamu bila kuwatia ndani wale wasiopaswa kuhusika.—2/15, ukurasa 7.

◻ Ni nini maana ya maneno ya Yesu “uzima ndani yenu,” yanayopatikana kwenye Yohana 6:53?

Katika Yohana sura ya 6 Yesu anaonyesha kuwa maneno “uzima wa milele” ni sawa na “uzima ndani yenu,” yaani, kuingia mwishowe katika ujazo wa uzima. “Kundi dogo” la warithi wa Ufalme wanaupata wanapofufuliwa kuingia katika mbingu, na “kondoo wengine” wanafanya hivyo baada ya mwisho wa utawala wa miaka elfu moja wa Kristo Yesu. (Ufunuo 20:4, 5) —2/15, makala ya pili ya funzo, mafungu 13-15.

◻ Ni kanuni gani inayokaziwa katika sehemu zote za kitabu cha Nehemia iliyo somo kwetu leo?

Ni kanuni ya kwamba “[Yehova] asipoijenga nyumba waijengao wafanya kazi bure.” (Zaburi 127:1) Leo, katika shughuli zetu zote, tutafanikiwa ikiwa tu tuna baraka ya Yehova.—2/15.

Ni jambo gani lililomtegemeza Ayubu wakati wa jaribu lake, na linaweza kutusaidiaje sisi leo?

Ayubu alikuwa na uhakika kwamba uzima sio uu huu tu. (Ayubu 14:13-15) Tukiwa na uhakika uo huo leo, kwamba Yehova atawafufua watumishi wake waaminifu, kunaweza kutusaidia tuelekeane na majaribu yo yote ambayo Shetani anaweza kuweka juu yetu. (Waebrania 6:10; 11:6)—3/1, makala ya pili ya funzo, mafungu 20.

◻ Wazazi wanaweza kujifunza somo gani juu ya matokeo ya dhambi ya Daudi na Bath-sheba?

Yehova alitoa rehema kumwelekea Daudi kwa sababu ya lile agano la Ufalme, hivyo akawaruhusu yeye na Bath-sheba waendelee kuishi. Lakini, mneni wa Yehova aliwaambia hivi: “Kwa sababu pasipo shaka umemtendea Yehova kwa madharau kwa kutenda jambo hili, pia mwana mwenyewe, ambaye umezaliwa sasa hivi, atakufa hakika.” (2 Samweli 12:14, NW ) Jambo hilo linapasa liwakazie wazazi kwamba mwenendo wao unaweza kuleta matokeo makubwa juu ya watoto wao,—3/15, ukurasa 31.

◻ Ni jambo gani linalotakwa ndipo mtu awe mshiriki anayekubaliwa wa Mashahidi wa Yehova? Ni lazima mtu huyo aukubali ujumla wote wa mafundisho ya Biblia, kutia na imani zile za Kimaandiko zinazofuatwa na Mashahidi wa Yehova peke yao.—4/1, ukurasa 31.

Ni lazima mtu huyo aukubali ujumla wote wa mafundisho ya Biblia, kutia na imani zile za Kimaandiko zinazofuatwa na Mashahidi wa Yehova peke yao.—4/1, ukurasa 31.

◻ Mawazo mabaya yakiingia katika akili zetu mara kwa mara, tufanye nini?

Inatupasa tukatae kuacha akili zetu zikae-kae zikifikiria mawazo hayo mabaya. Ili kutusaidia kufanya hivyo, imetupasa tumwendee Yehova katika sala bila kukawia, ‘tumtwike Yehova mzigo wetu.’ (Zaburi 55:22)—4/1, ukurasa 25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki