Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 5/15 kur. 8-9
  • Lile Swali la Ubaba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lile Swali la Ubaba
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Lile Swali la Ubaba
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Je, Baba yao Ni Abrahamu au Ni Ibilisi?
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Yehova Alimwita “Rafiki Yangu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Abrahamu Alikuwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 5/15 kur. 8-9

Maisha na Huduma ya Yesu

Lile Swali la Ubaba

WAKATI wa Sikukuu ya Mahema (Vibanda) ya 32 W.K., mazungumzo ya Yesu pamoja na viongozi wa kidini Wayahudi yanakuwa makali sana. “Mimi najua kwamba ninyi ni wazaliwa wa Abrahamu,” Yesu anakiri, “lakini ninyi mnatafuta kuniua mimi, kwa sababu neno langu halifanyi maendeleo miongoni mwenu ninyi. Mambo ambayo mimi nimeona pamoja na Baba yangu ninayanena; na ninyi, basi, mnafanya mambo ambayo ninyi mmesikia kutoka kwa baba yenu.”

Ingawa hatambulishi baba yao ni nani, Yesu anaelewesha wazi kwamba baba yao ni tofauti na yule wake. Bila kuwa na habari Yesu anamaanisha nani, viongozi wa kidini Wayahudi wanarudisha hivi: “Baba yetu ni Abrahamu.” Wao wanahisi kwamba wana imani ile ile kama Abrahamu, aliyekuwa rafiki ya Mungu.

Hata hivyo, Yesu anawashtua na jibu hili: “Ikiwa ninyi ni watoto wa Abrahamu, fanyeni kazi za Abrahamu.” Kweli kweli, mwana halisi huiga baba yake. “Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua mimi,” Yesu anasema, “mwanamume ambaye amewaambia ninyi ukweli ambao mimi nilisikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya hivi.” Kwa hiyo Yesu anasema tena: “Ninyi mnafanya kazi za baba yenu.”

Bado akili zao hazishiki Yesu anaongea juu ya nani. Wanashikilia kwamba wao ni wana halali wa Abrahamu, wakisema: “Sisi hatukuzaliwa kutokana na uasherati.” Kwa sababu hiyo, kwa kudai kwamba wao ni waabudu wa kweli kama Abrahamu, wanakazania hivi: “Sisi tuna Baba mmoja, Mungu.”

Lakini je! kweli Mungu ndiye Baba yao? “Kama Mungu angekuwa ndiye Baba yenu,” Yesu anarudisha, “ninyi mngenipenda mimi, kwa maana mimi nilitokeza na nipo hapa kutoka kwa Mungu. Wala mimi sikuja kwa uanzilishi wangu mwenyewe hata kidogo bali huyo Mmoja ndiye alinituma mimi. Kwa nini ninyi hamjui ninalonena?”

Yesu amejaribu kuonyesha hawa viongozi wa kidini matokeo ya wao kumkataa. Lakini sasa anasema hivi kwa kutoboa wazi: “Ninyi ni wa kutoka kwa baba yenu Ibilisi, na ninyi mnataka kufanya tamaa za baba yenu.” Ibilisi ni baba wa aina gani? Yesu alimtambulisha kuwa muuaji na pia akasema: “Yeye ni mwongo na baba ya ule uwongo.” Kwa hiyo Yesu anamalizia hivi: “Yeye ambaye ni wa kutoka kwa Mungu husikiliza semi za Mungu. Hii ndiyo sababu ninyi hamsikilizi, kwa sababu ninyi si wa kutoka kwa Mungu.”

Kwa kukasirishwa na shutumu la Yesu, Wayahudi wanajibu hivi: “Je! kwa kufaa sisi hatusemi, Wewe ni Msamaria na una roho mbaya?” Mtajo “Msamaria” unatumiwa kama usemi wa madharau na suto, Wasamaria wakiwa ni kikundi cha watu wanaochukiwa na Wayahudi.

Akipuuza lawama hilo lenye madharau kwamba ni Msamaria, Yesu anarudisha hivi: “Mimi sina roho mbaya, lakini mimi naheshimu Baba yangu, na ninyi mnanivunjia mimi heshima.” Akiendelea, Yesu anatoa ahadi hii ya kugutusha: “Ikiwa mtu ye yote anashika neno langu, yeye hataona kamwe kifo hata kidogo.” Bila shaka, Yesu hamaanishi kwamba wote wanaomfuata hawataona kamwe kifo kwa uhalisi. Bali, anamaanisha kwamba wao hawataona kamwe uharibifu wa milele, au “kifo cha pili,” ambacho hakina ufufuo.

Hata hivyo, Wayahudi wanachukua maneno ya Yesu kihalisi. Kwa sababu hiyo, wao wanasema: “Sasa sisi tunajua wewe una roho mbaya. Abrahamu alikufa, pia manabii; lakini wewe unasema, ‘Ikiwa mtu ye yote anashika neno langu, yeye hataonja kamwe kifo hata kidogo.’ Wewe si mkubwa kuliko Abrahamu baba yetu, ambaye alikufa, sivyo? Pia, manabii walikufa. Wewe unadai kuwa nani?”

Katika mazungumzo mazima haya, ni wazi kwamba Yesu anaonyesha wanaume hawa uhakika wa kwamba yeye ndiye Mesiya aliyeahidiwa. Lakini badala ya kujibu swali lao moja kwa moja juu ya yeye ni nani,

Yesu anasema: “Kama mimi najitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ndiye anayenitukuza mimi, yeye ambaye ninyi mnasema ndiye Mungu wenu; na bado ninyi mmekuwa hammjui. Lakini mimi namjua. Na kama mimi ningesema simjui ningepaswa kuwa kama ninyi, mwongo.” Akiendelea, Yesu anarejeza tena kwenye Abrahamu mwaminifu, akisema: “Abrahamu baba yenu alishangilia sana katika tazamio la kuona siku yangu, na yeye aliiona na kushangilia.” Ndiyo, kwa macho ya imani, Abrahamu alitazama mbele kwenye kuwasili kwa Mesiya aliyeahidiwa. Kwa kutoitikadi, Wayahudi wanarudisha hivi: “Wewe hujafika bado miaka hamsini, na bado wewe umeona Abrahamu?”

“Kwa ukweli sana mimi nawaambia ninyi,” Yesu anajibu, “kabla ya Abrahamu kuja kuwako, mimi nimekuwako.” Bila shaka, Yesu anarejeza kwenye kuwako kwake kabla ya kuwa binadamu akiwa mtu-roho mwenye uweza mbinguni.

Kwa kutiwa hasira kali na dai la Yesu kwamba alikuwako kabla ya Abrahamu, Wayahudi wanaokota mawe wamvurumishie. Lakini yeye anajificha na kwenda nje ya hekalu bila umizo. Yohana 8:37-59; Ufunuo 3:14; 21:8, NW.

♦ Yesu anaonyesha jinsi gani kwamba yeye na adui zake wana mababa tofauti?

♦ Ina maana gani Wayahudi kuita Yesu Msamaria?

y♦ Ni katika maana gani Yesu anamaanisha kwamba wafuasi wake hawataona kamwe kifo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki