-
Tumaini Hakika kwa WafuMtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
Itikio la Yesu kwa kifo cha Lazaro lafunua hisia nyororo sana za Mwana wa Mungu. Hisia zake zenye kina katika pindi hii zaonyesha waziwazi kutamani kwake sana kufufua wafu. Twasoma hivi: “Maria, alipowasili ambapo Yesu alikuwa naye alipomwona, alianguka penye miguu yake, akimwambia: ‘Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu asingalikufa.’ Kwa hiyo, Yesu alipomwona akitoa machozi na Wayahudi waliokuja pamoja naye wakitoa machozi, akapiga kite katika roho na kuwa mwenye kutaabika; naye akasema: ‘Mmemlaza wapi?’ Wakamwambia: ‘Bwana, njoo uone.’ Yesu akatokwa na machozi. Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kusema: ‘Ona, jinsi alivyokuwa na shauku naye!’”—Yohana 11:32-36, NW.
Huruma ya Yesu ya kuhisiwa moyoni inaonyesha hapa na mafungu haya matatu ya maneno: “akapiga kite,” “kuwa mwenye kutaabika,” na “akatokwa na machozi.” Maneno ya lugha ya awali yaliyotumiwa katika kuandika kisa hiki chenye kugusa moyo yaonyesha kwamba Yesu aliathiriwa sana na kifo cha rafiki yake mpendwa Lazaro na kumwona dada ya Lazaro akitoa machozi hivi kwamba macho Yake yalifurika machozi.a
Jambo la kutazamisha sana ni kwamba hapo awali Yesu alikuwa amewarudisha watu wengine wawili kwenye uhai. Na alikusudia kabisa kufanya vivyo hivyo na Lazaro. (Yohana 11:11, 23, 25) Hata hivyo, “akatokwa na machozi.” Basi, kurudisha wanadamu kwenye uhai, si utaratibu fulani tu wa Yesu. Hisia zake nyororo na zenye kina kama zilivyodhihirishwa kwenye pindi hii zaonyesha kwa wazi kutamani kwake sana kuondoa madhara ya kifo.
-
-
Tumaini Hakika kwa WafuMtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
a Neno la Kigiriki linalofasiriwa “akapiga kite” linatoka kwenye kitenzi (em·bri·maʹo·mai) kimaanishacho kuathiriwa sana, au kwa njia ya kuumiza. Msomi mmoja wa Biblia aonyesha hivi: “Hapa laweza kumaanisha tu kwamba Yesu alishikwa kwa nguvu na hisiamoyo yenye kina sana hivi kwamba kupiga kite kulitokezwa moyoni Mwake kwa lazima.” Usemi unaotafsiriwa “kuwa mwenye kutaabika” watokana na neno la Kigiriki (ta·rasʹso) lionyeshalo kufadhaika. Kulingana na mtunga-kamusi fulani, linamaanisha “kumsababishia mtu msukosuko wa kindani, . . . kuathiri kwa umivu au huzuni kubwa.” Usemi huu “akatokwa na machozi” watokana na kitenzi cha Kigiriki (da·kryʹo) kimaanishacho “kudondoa machozi, kutoa machozi kimyakimya.”
-