Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tunachochewa na “Mambo Yenye Fahari ya Mungu”
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Agosti 1
    • Wachochewa Kutenda!

      4. Ni unabii gani wa Yoeli uliotimizwa siku ya Pentekoste 33 W.K.?

      4 Mara tu baada ya kupokea roho takatifu, wanafunzi waliokuwa Yerusalemu walianza kuwatangazia wengine habari njema ya wokovu, wakianza na umati uliokuwa umekusanyika asubuhi siku hiyo. Mahubiri yao yalitimiza unabii wenye kutokeza, uliokuwa umeandikwa na Yoeli mwana wa Pethueli karne nane mapema: “Nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu . . . kabla haijaja hiyo siku ya BWANA iliyo kuu na itishayo.”—Yoeli 1:1; 2:28, 29, 31; Matendo 2:17, 18, 20.

      5. Wakristo wa karne ya kwanza walitabiri katika maana gani? (Ona kielezi-chini.)

      5 Je, hii ilimaanisha kwamba Mungu angetokeza manabii wa kiume na wa kike kama Daudi, Yoeli, na Debora, na kuwatumia kutabiri mambo ya wakati ujao? La. ‘Wana waume kwa wake, watumishi wanaume na wanawake’ Wakristo wangetabiri katika maana ya kwamba wangechochewa na roho ya Yehova kutangaza “mambo yenye fahari” ambayo Yehova alikuwa amefanya na ambayo bado angefanya. Kwa hiyo wangetumikia wakiwa wasemaji wa Aliye Juu Zaidi.a Hata hivyo, umati ulitendaje?—Waebrania 1:1, 2.

  • Tunachochewa na “Mambo Yenye Fahari ya Mungu”
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Agosti 1
    • a Yehova alipowachagua Musa na Aroni wakazungumze na Farao kwa niaba ya watu wake, Yeye alimwambia Musa hivi: ‘Nimekufanya wewe kuwa kama Mungu kwa Farao; na huyo ndugu yako Haruni atakuwa nabii wako.’ (Kutoka 7:1, italiki ni zetu.) Aroni alitumikia akiwa nabii, si kwa kutabiri mambo ya wakati ujao, bali kwa kuwa msemaji wa Musa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki