-
“Mtu Mwingine Hajapata Kamwe Kusema Kama Huyu”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
5. Toa mifano ya maneno yaliyosemwa na Yesu ambayo yalikuwa rahisi lakini yaliyojaa maana.
5 Alipofundisha, mara nyingi Yesu alitumia sentensi fupi zinazoeleweka kwa urahisi na kutumia maneno yaliyojaa maana. Nyakati hizo hakukuwa na vitabu vilivyochapishwa. Hivyo, kwa kutumia lugha ya kawaida, Yesu alikazia ujumbe wake katika akili na mioyo yao hivi kwamba hawangeweza kusahau. Fikiria mifano fulani: “Acheni kuhukumu ili msihukumiwe.” “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali wenye kuugua ndio wanaomhitaji.” “Roho inataka, lakini mwili ni dhaifu.” “Mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.” “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”b (Mathayo 7:1; 9:12; 26:41; Marko 12:17; Matendo 20:35) Maneno hayo yangali yanakumbukwa karibu miaka 2,000 baadaye.
-
-
“Mtu Mwingine Hajapata Kamwe Kusema Kama Huyu”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
b Maneno hayo ya mwisho yanayopatikana kwenye Matendo 20:35 yananukuliwa na mtume Paulo tu. Huenda alisimuliwa maneno hayo (na mtu aliyemsikia Yesu akiyasema au alisimuliwa na Yesu aliyefufuliwa) au aliyapokea kupitia ufunuo kutoka kwa Mungu.
-