-
Wakristo wa Mapema na Sheria ya MusaMnara wa Mlinzi—2003 | Machi 15
-
-
Namna Gani Wakristo Wayahudi?
12. Ni swali gani ambalo halikuwa limeshughulikiwa?
12 Baraza linaloongoza lilikuwa limeonyesha wazi kwamba haikuwa lazima Wakristo wasio Wayahudi watahiriwe. Lakini namna gani Wakristo Wayahudi? Washiriki wa baraza linaloongoza hawakuwa wameshughulikia swali hilo katika uamuzi wao.
13. Kwa nini lilikuwa kosa kusisitiza kwamba ilikuwa lazima kufuata Sheria ya Musa ili kuokolewa?
13 Baadhi ya Wayahudi Wakristo waliokuwa “wenye bidii kuhusu Sheria” waliendelea kuwatahiri watoto wao na kufuata matakwa fulani ya Sheria. (Matendo 21:20) Mbali na kutahiri watoto, wengine hata walisisitiza kwamba ni lazima Wakristo Wayahudi wafuate Sheria ili waokolewe. Walikuwa wamekosea sana kwa kufanya hivyo. Kwa mfano, Mkristo hangeweza kutoa dhabihu ya mnyama ili asamehewe dhambi. Dhabihu ya Kristo ilibatilisha dhabihu hizo. Namna gani takwa la Sheria kwamba Wayahudi wasishirikiane kwa ukaribu na watu wasio Wayahudi? Ingekuwa vigumu sana kwa waeneza-evanjeli wenye bidii kufuata matakwa hayo na bado waendelee na kazi yao ya kufundisha watu wasio Wayahudi mambo yote ambayo Yesu alikuwa amefundisha. (Mathayo 28:19, 20; Matendo 1:8; 10:28)a Hakuna uthibitisho kwamba jambo hilo lilifafanuliwa katika mkutano wa baraza linaloongoza. Hata hivyo, kutaniko halikuachwa bila msaada.
-
-
Wakristo wa Mapema na Sheria ya MusaMnara wa Mlinzi—2003 | Machi 15
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 24]
Paulo Akabili Jaribu kwa Unyenyekevu
Baada ya safari ya umishonari iliyofanikiwa, Paulo aliwasili Yerusalemu mwaka wa 56 W.K. Huko alipatwa na jaribu fulani. Habari zilikuwa zimefika kutanikoni kwamba alikuwa akifundisha ya kuwa Sheria ilikuwa imebatilishwa. Wanaume wazee walihofu kwamba Wakristo Wayahudi waliokuwa wamegeuzwa imani karibuni wangekwazwa na jinsi Paulo alivyozungumza waziwazi kuhusu Sheria na huenda wangekata kauli kwamba Wakristo hawakuheshimu mipango ya Yehova. Katika kutaniko, kulikuwa na Wakristo Wayahudi wanne waliokuwa wameweka nadhiri, labda ya kuwa Wanadhiri. Walipaswa kwenda hekaluni ili kukamilisha matakwa ya nadhiri hiyo.
Wanaume wazee walimwomba Paulo aende hekaluni pamoja nao na kugharimia mahitaji yao. Paulo alikuwa ameongozwa na roho ya Mungu kuandika angalau barua mbili ambapo alisema kwamba haikuwa lazima kushika Sheria ili kuokolewa. Hata hivyo, alijali dhamiri za wengine. Alikuwa ameandika hivi awali: “Kwa wale walio chini ya sheria nilipata kuwa kama aliye chini ya sheria . . . ili niweze kuwapata wale walio chini ya sheria.” (1 Wakorintho 9:20-23) Ingawa hakuachilia mambo wakati kanuni za Kimaandiko zilipohusika, Paulo aliona kwamba angeweza kukubaliana na maoni ya wanaume wazee. (Matendo 21:15-26) Hakukosea kufanya hivyo. Mpango wa nadhiri haukupingana na Maandiko, nalo hekalu lilitumiwa kwa ajili ya ibada safi wala si ibada ya sanamu. Ili asiwakwaze wengine, Paulo alikubaliana na ombi la wanaume hao wazee. (1 Wakorintho 8:13) Yaelekea Paulo alihitaji sifa ya unyenyekevu ili kufanya hivyo, jambo linalofanya tumheshimu hata zaidi.
-