-
“Nisikilizeni Ninapojitetea”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
17 Baadhi ya wale waliokuwa wamesimama hapo wakashangazwa—si na yule aliyempiga Paulo, bali na jibu la Paulo! Wakamuuliza: “Je, unamtukana kuhani mkuu wa Mungu?” Jibu la Paulo lilionyesha kwamba yeye ni mnyenyekevu na pia anaiheshimu Sheria. Alisema: “Akina ndugu, sikujua yeye ni kuhani mkuu. Kwa maana imeandikwa, ‘Usiseme vibaya juu ya mtawala wa watu wako.’”d (Mdo. 23:4, 5; Kut. 22:28) Paulo akabadili njia yake. Akijua kwamba washiriki wa mahakama hiyo ni Mafarisayo na Masadukayo, akasema: “Wanaume, akina ndugu, mimi ni Farisayo, mwana wa Mafarisayo. Ninahukumiwa kwa sababu ya tumaini la ufufuo wa wafu.”—Mdo. 23:6.
-
-
“Nisikilizeni Ninapojitetea”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
d Watu fulani wamesema kwamba inawezekana Paulo hakuwa akiona vizuri kwa hiyo hakumtambua kuhani mkuu. Au huenda alikuwa mbali na Yerusalemu kwa muda mrefu sana hivi kwamba hakumjua kuhani mkuu wa wakati huo. Au kwa sababu ya umati wa watu uliokuwapo labda Paulo hangeweza kuona ni nani aliyetoa amri apigwe.
-