Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • “Akiwahubiria Ufalme wa Mungu” (Mdo. 28:30, 31)

      19. Ni kwa njia gani Paulo alitumia hali zake vizuri?

      19 Luka anamalizia masimulizi yake kwa jambo lenye kutia moyo sana. Anasema hivi: “[Paulo] akakaa huko kwa miaka miwili kamili katika nyumba yake ya kukodi, naye alikuwa akiwakaribisha kwa fadhili wale wote waliomtembelea, akiwahubiria Ufalme wa Mungu na kuwafundisha kumhusu Bwana Yesu Kristo kwa uhuru mwingi wa kusema, bila kizuizi.” (Mdo. 28:30, 31) Hicho ni kielelezo kizuri sana cha ukarimu, imani, na bidii!

      20, 21. Taja watu mbalimbali walionufaika na huduma ya Paulo katika jiji la Roma.

      20 Mmoja wa watu waliopokewa na Paulo kwa fadhili ni Onesimo, mtumwa aliyetoroka Kolosai. Paulo alimsaidia Onesimo kuwa Mkristo, naye Onesimo akawa “ndugu . . . mwaminifu na mpendwa” kwa Paulo. Paulo anamwita “mwanangu . . . ambaye nimekuwa baba yake.” (Kol. 4:9; Flm. 10-12) Bila shaka Onesimo alimtia moyo sana Paulo!a

      21 Wengine pia walinufaika na mfano mzuri wa Paulo. Aliwaandikia hivi Wafilipi: “Hali yangu kwa kweli imesaidia kuendeleza habari njema, hivi kwamba vifungo vyangu vya gereza kwa ajili ya Kristo vimejulikana wazi kati ya Walinzi wote wa Mfalme na watu wengine wote. Sasa akina ndugu wengi katika Bwana wamekuwa na uhakika kwa sababu ya vifungo vyangu vya gereza, nao wanaonyesha uhodari mwingi wa kulisema neno la Mungu bila woga.”​—Flp. 1:12-14.

  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 25, 26. Paulo alijionea utimizo wa unabii gani miaka isiyozidi 30 baadaye, na hali hiyo inalingana jinsi gani na siku zetu?

      25 Mtume wa Kristo aliye katika kifungo cha nyumbani “akiwahubiria Ufalme wa Mungu” wote wanaomtembelea—mwisho wenye kutia moyo sana wa kitabu cha Matendo! Katika sura ya kwanza, tulisoma kuhusu mgawo ambao Yesu aliwapa wafuasi wake aliposema: “Roho takatifu itakapokuja juu yenu mtapokea nguvu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Sasa, miaka isiyozidi 30 baadaye, tayari ujumbe wa Ufalme ulikuwa umehubiriwa “katika uumbaji wote chini ya mbingu.”d (Kol. 1:23) Huo ni ushahidi mkubwa wa nguvu za roho ya Mungu!—Zek. 4:6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki