Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uwezo wa Kurudisha Hali Nzuri—Yehova ‘Anafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya’
    Mkaribie Yehova
    • 3. Ni taraja gani lenye kufariji linalotajwa kwenye Matendo 3:21, na Yehova atalitimizaje?

      3 Basi inafariji kama nini kujua kwamba Yehova ana uwezo wa kurudisha mambo yote katika hali nzuri! Kama tutakavyoona, Mungu ana uwezo wa kurudisha katika hali nzuri mambo mengi sana yaliyoharibika duniani. Kwa kweli, Biblia inaonyesha kwamba Yehova anakusudia ‘kurudisha mambo yote.’ (Matendo 3:21) Yehova atatumia Ufalme wa Kimesiya, unaotawaliwa na Mwanaye, Yesu Kristo ili kutimiza hayo. Kuna uthibitisho kwamba Ufalme huo ulianza kutawala mbinguni mwaka wa 1914.a (Mathayo 24:3-14) Ni mambo gani yatakayorudishwa katika hali nzuri? Tuchunguze baadhi ya mambo matukufu ambayo Yehova amenuia kurudisha katika hali nzuri. Tunaweza kuona na kufurahia mojawapo ya mambo hayo hivi sasa. Mambo mengineyo yatarudishwa kikamili wakati ujao.

  • Uwezo wa Kurudisha Hali Nzuri—Yehova ‘Anafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya’
    Mkaribie Yehova
    • a “Nyakati za kurudishwa kwa mambo yote” zilianza wakati Ufalme wa Kimesiya uliposimamishwa, mrithi wa Mfalme Daudi aliyekuwa mwaminifu alipowekwa kuwa mtawala wa Ufalme huo. Yehova alikuwa amemwahidi Daudi kwamba mrithi wake angetawala milele. (Zaburi 89:35-37) Lakini baada ya Babiloni kuharibu Yerusalemu mnamo mwaka wa 607 K.W.K., kiti cha enzi cha Mungu hakikukaliwa na mwanadamu mwingine yeyote aliye mzao wa Daudi. Yesu, aliyezaliwa duniani akiwa mrithi wa Daudi, akawa Mfalme aliyeahidiwa tangu kale alipotawazwa mbinguni.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki