-
Barnaba Yule “Mwana wa Faraja”Mnara wa Mlinzi—1998 | Aprili 15
-
-
Muda mfupi baada ya Pentekoste 33 W.K., Barnaba, aliyekuwa Mlawi kutoka Saiprasi, aliuza sehemu fulani ya shamba kwa kujitolea na kuwapa mitume hizo fedha. Kwa nini alifanya hivyo? Simulizi katika Matendo latuambia kwamba miongoni mwa Wakristo katika Yerusalemu wakati huo, “ugawanyaji ulikuwa ukifanywa kwa kila mmoja, kama vile alivyokuwa na uhitaji.” Barnaba kwa wazi aliona kwamba kulikuwa na uhitaji, naye alifanya jambo fulani kwa uchangamfu kuuhusu. (Matendo 4:34-37) Huenda ikawa alikuwa tajiri, lakini hakusita kutoa mali zake za kimwili na kujitoa mwenyewe kwa ajili ya kusongeza mbele masilahi ya Ufalme.b “Mahali popote ambako Barnaba alipata watu au hali zilizohitaji kitia-moyo, aliwapa wote kitia-moyo ambacho aliweza,” aonelea msomi F. F. Bruce. Hilo ni dhahiri kutokana na kisa cha pili ambamo yeye atajwa.
-
-
Barnaba Yule “Mwana wa Faraja”Mnara wa Mlinzi—1998 | Aprili 15
-
-
b Kwa kufikiria yale ambayo yalikuwa yamewekwa imara na Sheria ya Kimusa, watu fulani wameuliza jinsi Barnaba, Mlawi, alivyokuja kupata shamba. (Hesabu 18:20) Hata hivyo, lazima ijulikane kwamba, haieleweki kama hiyo mali ilikuwa Palestina au Saiprasi. Zaidi ya hilo, yawezekana kwamba ilikuwa tu kiwanja cha maziko ambacho Barnaba alikuwa amejipatia katika eneo la Yerusalemu. Hata iweje, Barnaba alitoa mali yake kuwasaidia wengine.
-