Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutaniko “Likaingia Katika Kipindi cha Amani”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 12 Anania aliukubali mgawo aliopewa naye akapata baraka. Namna gani wewe? Unatii amri ya kutoa ushahidi kikamili, hata ikiwa una mashaka fulani kuhusu mgawo wako? Kwa wengine, kwenda nyumba kwa nyumba na kukutana na watu wasiowafahamu huwatia wasiwasi. Wengine huona ni vigumu kuwahubiria watu katika sehemu za biashara, barabarani, au kupitia simu au barua. Anania aliushinda woga wake naye akapata pendeleo la kumsaidia Sauli kuipokea roho takatifu.b Anania alifanikiwa kwa sababu alimwamini Yesu na kumwona Sauli kama ndugu yake. Kama alivyofanya Anania, sisi pia tunaweza kushinda woga wetu, kwa kutambua kwamba Yesu ndiye anayeongoza kazi ya kuhubiri, kuwajali watu na kuwaona kuwa wanaweza kuwa ndugu zetu hata wale wanaoonekana kuwa wenye kutisha.​—Mt. 9:36.

  • Kutaniko “Likaingia Katika Kipindi cha Amani”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • b Kwa kawaida, zawadi za roho takatifu zilipitishwa kupitia mitume. Hata hivyo, katika hali hii isiyo ya kawaida, inaonekana Yesu alimwamuru Anania apitishe zawadi za roho takatifu kwa Sauli. Baada ya kugeuzwa imani, kwa muda fulani, Sauli alikuwa peke yake, mbali na wale mitume wengine 12. Hata hivyo, inaonekana kwamba aliendelea kuwa mtendaji katika kipindi hicho. Inaonekana kwamba Yesu alihakikisha Sauli amepata nguvu zinazohitajika ili kuutimiza mgawo wake wa kuhubiri.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki