-
1 | Usiwe na UbaguziMnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2022 | Na. 1
-
-
Biblia Inasema:
“Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa [kila] mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.”—MATENDO 10:34, 35.
Inamaanisha Nini?
Yehovaa Mungu hapimi thamani yetu kwa kutegemea taifa letu, jamii yetu, rangi ya ngozi yetu, au utamaduni wetu. Badala yake anakazia jambo la maana zaidi, yaani, jinsi tulivyo kwa ndani. Kwa kweli, “mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”—1 Samweli 16:7.
-