Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 | Usiwe na Ubaguzi
    Mnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2022 | Na. 1
    • Biblia Inasema:

      “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa [kila] mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.”​—MATENDO 10:34, 35.

      Inamaanisha Nini?

      Yehovaa Mungu hapimi thamani yetu kwa kutegemea taifa letu, jamii yetu, rangi ya ngozi yetu, au utamaduni wetu. Badala yake anakazia jambo la maana zaidi, yaani, jinsi tulivyo kwa ndani. Kwa kweli, “mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”​—1 Samweli 16:7.

  • 1 | Usiwe na Ubaguzi
    Mnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2022 | Na. 1
    • Mwanzoni, Titus alipambana kuondoa chuki moyoni mwake. Anasema hivi: “Ilikuwa vigumu sana kubadili njia yangu ya kufikiri na kutenda.” Lakini, andiko la Matendo 10:34, 35 linaloeleza kwamba Mungu hana ubaguzi lilimsaidia kushinda chuki.

      Alipata matokeo gani? Titus anasema: “Nilikuja kusadiki kwamba Mashahidi wa Yehova ndio wanaofuata dini ya kweli wakati nilipoona waziwazi jinsi walivyopendana, bila kujali rangi au jamii yao. Hata kabla sijabatizwa na kuwa Shahidi, mshiriki mmoja wa kutaniko ambaye ni mzungu alinialika nyumbani kwake kwa ajili ya chakula. Ilikuwa kama ndoto. Mbali na kula chakula nyumbani kwake, sikuwa nimewahi kamwe kuketi hivyo kwa amani pamoja na mzungu. Sasa nilikuwa mshiriki wa undugu wa kweli wa ulimwenguni pote.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki