Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp22 Na. 1 kur. 6-7
  • 1 | Usiwe na Ubaguzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 1 | Usiwe na Ubaguzi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema:
  • Inamaanisha Nini?
  • Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:
  • Tito—“Mfanyakazi Mwenzi kwa Ajili ya Masilahi Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Tito Anashughulika na Mgawo Mgumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kitabu cha Biblia Namba 56—Tito
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • 3 | Ondoa Chuki Akilini Mwako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
wp22 Na. 1 kur. 6-7
Mwanamume mweusi akiwa ameshika picha ya mwanamume mzungu anayetabasamu, na mwanamume mzungu akiwa ameshika picha ya mwanamume mweusi anayetabasamu. Nyuma ni picha za watu walio na hasira.

JINSI YA KUSHINDA CHUKI

1 | Usiwe na Ubaguzi

Biblia Inasema:

“Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa [kila] mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.”​—MATENDO 10:34, 35.

Inamaanisha Nini?

Yehovaa Mungu hapimi thamani yetu kwa kutegemea taifa letu, jamii yetu, rangi ya ngozi yetu, au utamaduni wetu. Badala yake anakazia jambo la maana zaidi, yaani, jinsi tulivyo kwa ndani. Kwa kweli, “mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”​—1 Samweli 16:7.

Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:

Ingawa hatuwezi kusoma mioyo ya watu, tunaweza kujitahidi kumwiga Mungu kwa kutowabagua wengine. Jitahidi kuona sifa za mtu binafsi badala ya kufikiri ni mtu mbaya kwa sababu anatokea katika jamii fulani. Ukitambua kwamba una hisia zisizofaa kuelekea watu wengine​—labda kwa sababu ya jamii au taifa lao—​sali kwa Mungu na umwombe akusaidie kung’oa hisia hizo. (Zaburi 139:23, 24) Ukimwomba Yehova kwa unyoofu akupe nguvu za kushinda ubaguzi, uwe na uhakika kwamba atasikiliza sala yako na kukusaidia.​—1 Petro 3:12.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi 83:18.

“Sikuwa nimewahi kamwe kuketi hivyo kwa amani pamoja na mzungu. Sasa nilikuwa mshiriki wa undugu wa kweli wa ulimwenguni pote.”​—TITUS

Simulizi la Maisha​—TITUS

Alishinda Chuki

Titus.

Titus alishirikiana na kikundi cha wahalifu ambao walikasirishwa sana na sheria za kibaguzi zilizowakandamiza watu. Anasema: “Tulikuwa tukienda mjini katika sehemu ambazo watu weusi hawakuruhusiwa kuingia, kama vile hoteli na vilabu vya pombe, ili tu kuanzisha vita.” Titus anakiri kwamba alifanya hivyo kwa sababu ya chuki. Anaendelea kusema hivi: “Nilipoanza kubishana na mtu fulani, iwe mwanamume au mwanamke, sikuzote nilikuwa wa kwanza kutupa ngumi.”

Titus alibadilika alipoanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Aliposoma Biblia, alibadili maoni yake. Alivutiwa hasa na ahadi ya wakati ujao ambapo “kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”​—Ufunuo 21:3, 4.

Mwanzoni, Titus alipambana kuondoa chuki moyoni mwake. Anasema hivi: “Ilikuwa vigumu sana kubadili njia yangu ya kufikiri na kutenda.” Lakini, andiko la Matendo 10:34, 35 linaloeleza kwamba Mungu hana ubaguzi lilimsaidia kushinda chuki.

Alipata matokeo gani? Titus anasema: “Nilikuja kusadiki kwamba Mashahidi wa Yehova ndio wanaofuata dini ya kweli wakati nilipoona waziwazi jinsi walivyopendana, bila kujali rangi au jamii yao. Hata kabla sijabatizwa na kuwa Shahidi, mshiriki mmoja wa kutaniko ambaye ni mzungu alinialika nyumbani kwake kwa ajili ya chakula. Ilikuwa kama ndoto. Mbali na kula chakula nyumbani kwake, sikuwa nimewahi kamwe kuketi hivyo kwa amani pamoja na mzungu. Sasa nilikuwa mshiriki wa undugu wa kweli wa ulimwenguni pote.”

Ili ujue mengi zaidi kuhusu simulizi la Titus, soma gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1, 2009, ukurasa wa 28-29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki