Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • si kur. 239-241
  • Kitabu cha Biblia Namba 56—Tito

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu cha Biblia Namba 56—Tito
  • “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • YALIYOMO KATIKA TITO
  • KWA NINI NI CHENYE MAFAA
  • Tito Anashughulika na Mgawo Mgumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Tito—“Mfanyakazi Mwenzi kwa Ajili ya Masilahi Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Kaeni Wenye Afya Katika Imani!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Fanya Fundisho Lenye Afya Liwe Njia Yako ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
si kur. 239-241

Kitabu cha Biblia Namba 56—Tito

Mwandikaji: Paulo

Mahali Kilipoandikiwa: Makedonia (?)

Uandikaji Ulikamilishwa: c. (karibu) 61-64 W.K.

1. (a) Tito alikabidhiwa kazi gani? (b) Makundi katika Krete yalikuwa yametokea katika mazingira gani, nao Wakristo katika Krete walihitaji kufanya nini?

“PAULO, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo . . . kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tuishirikiyo.” (Tito 1:1, 4) Ndivyo ianzavyo barua ya Paulo kwa mfanya kazi mwenzake na mshirika wa muda mrefu Tito, ambaye yeye alikuwa amemwacha kwenye kisiwa cha Krete kupanga kitengenezo makundi vizuri zaidi. Tito alikuwa na kazi kubwa mikononi mwake. Kisiwa hiki, kilichosemwa kwamba kilikuwa ndiyo makao ya kale ya “baba wa miungu na wanadamu,” kilikuwa ndicho chanzo cha ule usemi, “Kukretisha Mkrete,” maana yake “kumzidi mlaghai kwa akili.”a Kukosa kusema ukweli kwa watu wa kisiwa hicho kulifanya tabia hiyo kuwa uneni wa kawaida, hivi kwamba Paulo hata alinukuu nabii wao mwenyewe kuwa akisema hivi: “Wakrete ni waongo sikuzote, hayawani wabaya, walafi wavivu.” (1:12) Wakrete wa siku ya Paulo pia wameelezwa kuwa kama ifuatavyo: “Tabia ya watu hawa ilikuwa ya kutokuwa na uthibitifu, kutokuwa na weupe wa moyo, na ya ugomvi-ugomvi; walikuwa watu wa pupa, upotovu, ubandia, na ulevi, kwa kadiri isiyo ya kikawaida; na Wayahudi waliokuwa wamekaa miongoni mwao waonekana kuwa waliwapita wenyeji katika ukosefu wa adili.”b Ilikuwa ni katika mazingira ya jinsi hiyo hasa kwamba makundi ya Krete yakatokea; na kwa hiyo ilihitajiwa kwa njia ya wazi kwamba waamini ‘wakatae katakata kutokumcha Mungu na tamaa za kilimwengu na waishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na ujitoaji kimungu,’ kama Paulo alivyohimiza.—2:12, NW.

2, 3. (a) Tito alikuwa na ushirika gani pamoja na Paulo? (b) Yaelekea Paulo alikuwa wapi alipomwandikia Tito, na kwa kusudi gani?

2 Kitabu cha Tito chenyewe hutoa habari chache sana juu ya ushirika wa Paulo na Tito. Kutokana na marejezo kwa Tito katika barua nyinginezo za Paulo, habari nyingi zaweza kupatikana. Tito, aliyekuwa Mgiriki, aliandamana mara nyingi na Paulo na angalau katika pindi moja alipanda kwenda Yerusalemu pamoja naye. (Gal. 2:1-5) Paulo humrejezea kuwa “mshirika wangu, na mtenda kazi pamoja nami.” Tito ndiye Paulo alikuwa amemtuma kwenda Korintho baada ya kuandika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho akiwa Efeso. Wakati aliokuwa katika Korintho, Tito alihusiana na mchango uliokuwa ukifanywa kwa ajili ya akina ndugu katika Yerusalemu, na baada ya hapo alirudi huko kwa mwelekezo wa Paulo ili akamalize mchango huo. Ilikuwa ni katika safari ya kurudi Korintho kutoka kwenye mkutano wake na Paulo katika Makedonia kwamba Tito alitumiwa kupeleka barua ya pili kutoka kwa Paulo iwaendee Wakorintho.—2 Kor. 8:16-24; 2:13; 7:5-7.

3 Baada ya kuachiliwa kwake kutoka kifungo chake cha kwanza gerezani katika Rumi, Paulo alishirikiana tena na Timotheo na Tito wakati wa miaka ya mwisho ya huduma yake. Hii yaonekana kuwa ilihusisha utumishi katika Krete, Ugiriki, na Makedonia. Hatimaye, Paulo anenwa kuwa akienda Nikopoli, katika Ugiriki ya kaskazini-magharibi, ambako yaonekana alikamatwa na kupelekwa Rumi ili kufungwa gerezani mara yake ya mwisho na kuuawa. Ilikuwa ni wakati wa ziara ya Krete kwamba Paulo akawa amemwacha Tito huko ‘asahihishe mambo yaliyokuwa na kasoro na kuweka wanaume wazee katika jiji baada ya jiji,’ kupatana na maagizo aliyokuwa amempa Tito. Yaonekana barua ya Paulo iliandikwa muda mfupi baada ya yeye kumwacha Tito katika Krete, ikielekea sana kuwa iliandikiwa Makedonia. (Tito 1:5, NW; 3:12; 1 Tim. 1:3; 2 Tim. 4:13, 20) Yaonekana kuwa ilitimiza kusudi kama lile la Timotheo wa Kwanza, yaani, kumtia moyo mfanya kazi mwenzi wa Paulo na kumpa utegemezo wenye mamlaka katika wajibu wake mbalimbali.

4. Ni lazima barua kwa Tito iwe iliandikwa wakati gani, na ni nini uthibitisho wa uasilia wayo?

4 Ni lazima iwe Paulo aliandika barua hiyo wakati fulani kati ya kufungwa gerezani kwake kwa kwanza na kwa pili kule Rumi, au karibu 61 mpaka 64 W.K. Uzito wa uthibitisho wa uasilia wa barua kwa Tito ni kama ule ule wa zile barua kwa Timotheo zilizoandikwa muda uo huo, mara nyingi barua tatu hizo zikiitwa “barua za kiuchungaji” za Paulo. Mtindo wa kuandika wafanana. Irenaeus na Origen wote wawili wanukuu kutokana na Tito, na pia wajuzi wengine wengi wa kale watoa ushuhuda juu ya kukubaliwa kwa kitabu hiki. Hicho hupatikana katika Hati-mkono Sinaitic na Alexandrine. Katika Maktaba ya John Rylands mna kipande cha funjo, P32, ambacho ni ukurasa wa kodeksi ya karibu karne ya tatu W.K. kinatia ndani Tito 1:11-15 na 2:3-8.c Hakuna shaka kwamba kitabu hiki ni sehemu asilia ya Maandiko yaliyopuliziwa na Mungu.

YALIYOMO KATIKA TITO

5. (a) Ni sifa gani za waangalizi ambazo Paulo akazia, na kwa nini hilo lahitajiwa? (b) Kwa nini ni lazima Tito akaripie kwa ukali, na ni nini lasemwa juu ya watu waliotiwa uchafu?

5 Waangalizi kuhimiza kwa fundisho lenye afya (1:1-16). Baada ya salamu yenye shauku, Paulo apangilia sifa za waangalizi. Yakaziwa kwamba ni lazima mwangalizi awe “asiyeshtakiwa neno,” mpenda wema, mwadilifu, mwenye uaminifu-mshikamanifu, “akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.” Hilo lahitajiwa kwa sababu ya “wadanganyaji” ambao hata wanapindua nyumba nzima-nzima kwa ajili ya pato lisilo la kufuata haki. Kwa hiyo ni lazima Tito ‘awakemee kwa ukali, ili wapate kuwa wazima katika imani; wasisikilize hadithi za Kiyahudi.’ Huenda watu waliochafuliwa wakajulisha rasmi peupe kwamba wao wamjua Mungu, lakini wao wamkana kwa kazi zao za kutotii.—1:6-10, 13, 14.

6. Ni ushauri gani ambao watolewa juu ya mwenendo wa Kikristo?

6 Kuishi kwa utimamu wa akili, uadilifu, na ujitoaji kimungu (2:1–3:15). Wanaume wenye umri mkubwa na wanawake wenye umri mkubwa wapaswa kuwa wazito na wenye hofu. Wanawake wachanga zaidi wapaswa kupenda waume zao na watoto wao na kujinyenyekeza kwa waume zao “ili neno la Mungu lisitukanwe.” Wanaume wachanga zaidi wapaswa kuwa kielelezo cha kazi nzuri na uneni wenye mafaa. Watumwa walio katika unyenyekeo wapaswa kuonyesha “uaminifu mwema wote.” Fadhili zisizostahiliwa za Mungu, zinazoongoza kwenye wokovu, zimedhihirishwa, zikitia moyo utimamu wa akili, uadilifu, na ujitoaji kimungu katika wale ambao Mungu amesafisha sana kupitia Kristo Yesu ili wawe ‘watu wa milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.’—2:5, 10, 14.

7. Paulo akazia nini kuhusiana na unyenyekevu, wokovu, na matendo mema?

7 Paulo akazia uhitaji wa kuzinyenyekea na kuzitii serikali na wa ‘kuonyesha upole wote kwa watu wote.’ Wakati mmoja Paulo na Wakristo wenzake walikuwa wabaya kama watu wengine. Si kutokana na kazi zozote zao wenyewe, bali kwa sababu ya fadhili za Mungu, upendo, na rehema, wao wameokolewa kwa njia ya roho takatifu na wamekuwa warithi kwenye tumaini la uhai wa milele. Kwa hiyo wale ambao huamini Mungu wapaswa “wakumbuke kudumu katika matendo mema.” Yawapasa kuepuka kabisa maswali ya kipumbavu na ugomvi juu ya Sheria, na kwa habari ya mtu ambaye aendeleza farakano, yawapasa kumkataa baada ya onyo la kwanza na la pili. Paulo amwomba Tito amjie kule Nikopoli na, baada ya kutoa maagizo mengine ya umisionari, akazia tena uhitaji wa kazi zilizo nzuri, ili kusiwe na ukosefu wa kuzaa matunda.—3:2, 7, 8.

KWA NINI NI CHENYE MAFAA

8. Ni nini katika shauri la Paulo kwenye barua kwa Tito kilicho ‘chema na chenye faida’ kwa ajili yetu leo, na kwa nini?

8 Wakristo Wakrete waliishi katika mazingira ya kusema uwongo, ufisadi, na pupa. Je! wafuatane tu na umati? Au je! wapaswa kuchukua hatua za wazi za kujitenga kabisa ili watumikie wakiwa watu waliotakaswa kwa Yehova Mungu? Kwa kujulisha kupitia Tito kwamba Wakrete wapaswa ‘kukumbuka kudumu katika matendo mema,’ Paulo alisema hivi: “Hayo ni mazuri, tena yana faida kwa wanadamu.” Ni “mazuri, tena yana faida” leo pia, katika ulimwengu ambao umezama katika tope la ukosefu wa ukweli na mazoea yasiyofuata haki, ambamo Wakristo halisi ‘hujifunza kudumu katika matendo mema,’ wakiwa wenye kuzaa katika utumishi wa Mungu. (3:8, 14) Laana kali yote ya Paulo juu ya ukosefu wa adili na uovu uliotisha makundi katika Krete ni onyo kwetu sasa ambapo ‘neema ya Mungu yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; na kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa.’ Wakristo pia wapaswa kuwa “tayari kwa kila kazi njema” katika kuonyesha utii kwa serikali, kudumisha dhamiri njema.—2:11, 12; 3:1.

9. Umaana wa fundisho la haki wakaziwaje, hasa ukiwa ni daraka la mwangalizi?

9 Tito 1:5-9 hukamilisha 1 Timotheo 3:2-7 katika kuonyesha yale ambayo roho takatifu hutaka kwa waangalizi. Hilo latia mkazo juu ya mwangalizi ‘kushika lile neno la imani’ na kuwa mwalimu katika kundi. Jinsi hilo lilivyo la lazima ili kuleta wote kwenye ukomavu! Kwa kweli, uhitaji huo wa fundisho la haki wakaziwa mara kadhaa katika barua kwa Tito. Paulo aonya Tito kwa upole aendelee ‘kunena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima.’ Wanawake wenye umri mkubwa wapaswa kuwa “wafundishao mema,” na watumwa wapaswa ‘kupamba mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.’ (Tito 1:9; 2:1, 3, 10) Akikazia uhitaji wa Tito akiwa mwangalizi kuwa imara na asiyehofu katika fundisho lake, Paulo asema hivi: “Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote.” Na kwa habari ya wale wanaokosa kutii, yeye asema hivi: “Uwakemee kwa ukali, ili wapate kuwa wazima katika imani.” Kwa hiyo, barua ya Paulo kwa Tito hasa ‘yafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki.’—Tito 2:15; 1:13; 2 Tim. 3:16.

10. Barua kwa Tito yatutia moyo kwenye nini, nayo yachochea msisimuo kwenye tumaini gani lenye furaha?

10 Barua kwa Tito husisimua uthamini wetu kwa ajili ya fadhili zisizostahilika za Mungu na hututia moyo tugeuke kutoka kwa kukaidi Mungu kwa ulimwengu ‘huku tukilingojea tumaini lenye furaha na udhihirisho mtukufu wa yule Mungu mkuu na wa Mwokozi wetu, Kristo Yesu.’ Kwa kufanya hivyo, wale waliojulishwa rasmi kuwa waadilifu kupitia Kristo Yesu waweza kuwa “warithi wa uzima wa milele” katika Ufalme wa Mungu.—Tito 2:13, NW; 3:7, UV.

[Maelezo ya Chini]

a Cyclopedia ya McClintock na Strong, chapa-mrudio ya 1981, Buku la 2, uurasa 564; The New Schaff-Herzog Encycopedia of Religious Knowledge, 1958, Buku 3, ukurasa 30

b Cyclopedia ya McClintock na Strong, Chapa-mrudio ya 1981, Buku 10, ukurasa 442.

c The Text of the New Testament, cha Kurt na Barbara Aland, kilichotafsiriwa na E. F. Rhodes, 1987, ukurasa 98.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki