Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 2/15 uku. 22
  • Kaeni Wenye Afya Katika Imani!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kaeni Wenye Afya Katika Imani!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Nini Kinatakwa kwa Waangalizi?
  • Tumia Fundisho Lenya Afya
  • Kitabu cha Biblia Namba 56—Tito
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Fanya Fundisho Lenye Afya Liwe Njia Yako ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Tito Anashughulika na Mgawo Mgumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Tito—“Mfanyakazi Mwenzi kwa Ajili ya Masilahi Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 2/15 uku. 22

Kaeni Wenye Afya Katika Imani!

Mambo Makuu Kutoka Tito

MAKUNDI ya Kikristo katika kisiwa cha Krete cha Mediterrania yalihitaji uangalifu wa kiroho. Nani angeweza kuyasaidia? Tito mfanya-kazi-mwenzi wa Mtume Paulo angeweza! Yeye alikuwa mwenye moyo mkuu, alistahili kufundisha, alikuwa mwenye bidii kwa kazi nzuri, na mwenye afya katika imani.

Paulo alizuru Krete kati ya kufungwa kwake kwa kwanza na kwa pili katika Roma. Alimwacha Tito nyuma katika kisiwa ili asahihishe mambo fulani na kuweka wazee wa kundi. Tito angehitajiwa pia kukaripia walimu bandia na kuweka mfano mzuri. Yote hayo yanafunuliwa katika barua ya Paulo kwa Tito, ambayo yawezekana ilipelekwa kutoka Makedonia kati ya 61 na 64 W.K. Kutumia shauri la mtume kwaweza kusaidia waangalizi wa ki-siku-hizi na waamini wenzao wawe wenye moyo mkuu, wenye bidii, na wenye afya kiroho.

Nini Kinatakwa kwa Waangalizi?

Ilihitajiwa sana kuweka waangalizi na kushughulika na matatizo fulani. (1:1-16) Ili awekwe kama mwangalizi, mtu alihitaji kuwa asiye na shtaka, mwenye mfano mzuri kibinafsi na katika maisha yake ya familia, mkaribishaji wa wageni, mwenye kusawazika, na mwenye kujidhibiti. Alihitaji kufundisha yaliyo kweli na kuhimiza na kukaripia wale wanaoonyesha maoni ya kupinganisha. Moyo mkuu ulihitajiwa kwa sababu wanaume wasiofuata utaratibu katika kundi wahitaji kunyamazishwa. Hiyo ilikuwa muhimu hasa kwa wale walioshikilia sana tohara, kwa maana walikuwa wamepindua nyumba nzima nzima. Karipio zito lingehitajiwa sana ikiwa makundi yangebaki katika afya ya kiroho. Leo, waangalizi Wakristo wanahitaji pia kuwa na moyo mkuu ili kutoa karipio na himizo, wakiwa na maoni ya kujenga kundi.

Tumia Fundisho Lenya Afya

Tito alitakiwa kutoa fundisho lenye afya ya kiroho. (2:1-15, NW) Wanaume wazee wangekuwa mifano katika kiasi, uzito, utimamu wa akili, imani, upendo, na uvumilivu. Wanawake wazee wangekuwa na “mwenendo wa kumwogopa Mungu.” Wakiwa “walimu wa yaliyo mema” wangeweza kuwasaidia wanawake vijana wawe na maoni yanayofaa kuhusu wajibu wao wakiwa wake na akina mama. Wanaume vijana wangekuwa timamu katika akili, na watumwa wangekuwa wamejitiisha kwa wenyeji wao kwa njia ambayo ingepamba fundisho la Mungu. Wakristo wote wangekataa katakata hali ya kumkana Mungu na kuishi kwa utimamu wa akili katika mfumo huu wa mambo wakingojea kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu na kwa Yesu Kristo, “ambaye alijitoa kwa ajili yetu ili atuokoe na kila aina ya uvunjaji wa sheria na kusafisha kwa ajili yake watu walio wake hasa, wenye bidii kwa ajili ya kazi njema.” Kwa kutumia shauri lenye afya kama hilo, sisi pia na ‘tupambe neno la Mungu.’

Shauri la kufunga la Paulo huendeleza afya ya kiroho. (3:1-15) Inahitajiwa sana kuonyesha utii unaofaa kwa watawala na kukuza wepesi wa kukubali maoni ya wengine. Wakristo wana tumaini la uhai wa milele, na maneno ya Paulo yangekaziwa ili kuwatia moyo kuweka akili zao kwenye kazi njema. Maswali ya upuzi na vita juu ya sheria vingeepukwa, na mwendelezi wa farakano angekataliwa baada ya kuonywa kwa upole mara mbili. Wazee wanapotumia shauri kama hilo leo, wao na waamini wenzao watakaa wakiwa wenye afya katika imani.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 22]

Kutofanywa Watumwa wa Divai: Ingawa ni lazima wanawake wasiwafundishe wanaume kundini, akina dada wenye umri mkubwa zaidi wanaweza kuwafunza wanawake wenye umri mdogo zaidi faraghani. Lakini ili wawe na matokeo mazuri kuhusu hilo, ni lazima wanawake wazee waangalie maneno ya Paulo: “Wanawake wazee na wawe na mwenendo wa kumwogopa Mungu, si wachongezi, wala wenye kufanywa watumwa wa divai nyingi mno, walimu wa yaliyo mema.” (Tito 2:1-5, NW; 1 Timotheo 2:11-14) Kwa sababu ya kufikiria matokeo ya kunywa, ni lazima waangalizi, watumishi wa huduma, na wanawake wa umri mkubwa zaidi wawe wenye kiasi, wasiwe wenye kujitoa wenyewe kwa divai nyingi. (1 Timotheo 3:2, 3, 8, 11) Ni lazima Wakristo wote waepuke ulevi na wanahitaji kujizuia kunywa vileo wakati wa kufanya ile “kazi takatifu” ya kuhubiri habari njema.—Warumi 15:16, NW; Mithali 23:20, 21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki