Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp22 Na. 1 kur. 10-11
  • 3 | Ondoa Chuki Akilini Mwako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 3 | Ondoa Chuki Akilini Mwako
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema:
  • Inamaanisha Nini?
  • Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:
  • Stefano—“Amejaa Kibali cha Mungu na Nguvu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Stefano Anapigwa kwa Mawe
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Jinsi ya Kushinda Chuki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
  • Tunaweza Kushinda Chuki!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
wp22 Na. 1 kur. 10-11
Mwanamume akiwazia anasalimiana na mtu wa jamii nyingine. Vivuli vyao vinaonyesha wameshika mabango katika maandamano huku wakiwa wanabishana.

JINSI YA KUSHINDA CHUKI

3 | Ondoa Chuki Akilini Mwako

Biblia Inasema:

“Mgeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mjihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.”​—WAROMA 12:2.

Inamaanisha Nini?

Mambo tunayowaza ni muhimu kwa Mungu. (Yeremia 17:10) Tunahitaji kufanya mengi zaidi ya kuepuka kusema au kufanya jambo linaloonyesha kwamba tuna chuki. Chuki huanzia akilini na moyoni. Hivyo, tunapaswa kuondoa dalili yoyote ya chuki akilini na moyoni. Tukifanya hivyo tutakuwa ‘tumegeuzwa’ kikweli na kushinda chuki.

Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:

Chunguza kwa unyoofu mawazo na hisia zako kuelekea watu wengine​—hasa wa jamii au taifa lingine. Jiulize: ‘Ninawaonaje? Je, maoni yangu yanategemea mambo ninayojua kuwahusu? Au ni ya kibaguzi?’ Epuka mitandao ya kijamii, filamu, au burudani zinazoonyesha chuki na jeuri.

Neno la Mungu linaweza kutusaidia kuondoa chuki moyoni na akilini

Si rahisi sikuzote kuwa wanyoofu tunapochunguza mawazo na hisia zetu. Lakini Neno la Mungu linaweza kutusaidia “kutambua fikira na makusudio ya moyo.” (Waebrania 4:12) Hivyo, endelea kuchunguza Biblia. Linganisha mafundisho yake na mawazo yako, na ujitahidi kupatanisha mawazo yako na mambo ambayo Biblia inafundisha. Neno la Mungu linaweza kutusaidia kushinda chuki inayoweza kuwa kama “ngome [yenye] nguvu” katika akili na moyo wetu.​—2 Wakorintho 10:4, 5.

Simulizi la Maisha​—STEPHEN

Alibadili Mawazo Yake

Stephen.

Stephen na familia yake waliteseka kwa sababu ya kuchukiwa na wazungu. Matokeo ni kwamba, alijiunga na kikundi cha kisiasa kilichotumia mbinu za kijeshi ili kupigania haki za raia. Baada ya muda, alishiriki kwenye matukio ya uhalifu yaliyochochewa na chuki. Stephen anasema: “Pindi moja mimi na rafiki zangu tulitazama filamu iliyoonyesha jinsi watumwa wa Kiafrika walivyoteswa nchini Marekani. Tukiwa tumekasirika kutokana na ukosefu huo wa haki, tuliwashambulia vijana wazungu waliokuwa katika jumba hilo la sinema. Kisha, tulienda katika maeneo ambayo wazungu waliishi ili kutafuta watu zaidi wa kuwapiga.”

Maoni ya Stephen yalibadilika kabisa alipoanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Kwa sababu nililelewa katika eneo lililokuwa na ubaguzi wa kijamii, nilishangazwa na jinsi Mashahidi walivyojiendesha. Kwa mfano, Shahidi mzungu alipotaka kwenda nchi nyingine, angewaacha watoto wake watunzwe na familia ya watu weusi. Pia, familia moja ya wazungu ilikubali kuishi na kijana mweusi aliyekosa makao.” Stephen alisadiki kabisa kwamba Mashahidi wa Yehova wana upendo wa kindugu ambao Yesu alitabiri ungewatambulisha Wakristo wa kweli.​—Yohana 13:35.

Ni nini kilichomsaidia Stephen kuacha matendo yaliyochochewa na chuki? Andiko la Waroma 12:2 lilimsaidia. Anasema: “Nilianza kutambua kwamba ninahitaji kubadili mtazamo wangu. Nilihitaji kutambua kwamba ninapaswa kutenda kwa njia ya amani na pia kuona kwamba hiyo ndiyo njia bora ya maisha.” Stephen amefurahia maisha bila kuwa na hisia za chuki kwa zaidi ya miaka 40 sasa.

Ili ujue mengi zaidi kuhusu simulizi la Stephen, soma gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 2015, ukurasa wa 10-11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki