Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp22 Na. 1 kur. 8-9
  • 2 | Usilipize Kisasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 2 | Usilipize Kisasi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema:
  • Inamaanisha Nini?
  • Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kulipiza Kisasi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Wakati Mtu Anapokuudhi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Nilikuwa Mjeuri na Mwenye Uchungu Moyoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Je! Kisasi Ni Kibaya?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
wp22 Na. 1 kur. 8-9
Wanaume wawili wenye hasira wakiwa wamekaa juu ya matawi ya mti. Kila mmoja wao anakata tawi alilokalia.

JINSI YA KUSHINDA CHUKI

2 | Usilipize Kisasi

Biblia Inasema:

“Msimlipe yeyote uovu kwa uovu. . . . Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, fanyeni amani na watu wote. Msijilipizie kisasi, . . . kwa maana imeandikwa: ‘“Kisasi ni changu; mimi nitalipa,” asema Yehova.’”​—WAROMA 12:17-19.

Inamaanisha Nini?

Ingawa ni kawaida kukasirika tunapokosewa, Mungu hataki tulipize kisasi. Badala yake anatusihi tumsubiri yeye kwa sababu hivi karibuni ataondoa ukosefu wote wa haki.​—Zaburi 37:7, 10.

Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:

Wanadamu wasio wakamilifu wanapolipiza kisasi, wanasababisha chuki. Kwa hiyo, mtu anapokukasirisha au kukuumiza, usilipize kisasi. Jitahidi kujibu kwa upole na ujizuie. Katika hali fulani, huenda ni vizuri kupuuza jambo lililotokea. (Methali 19:11) Lakini ukiona kuna ulazima wa kutoa taarifa kuhusu jambo hilo, unaweza kufanya hivyo. Kwa mfano, ikiwa umefanyiwa uhalifu, unaweza kuamua kutoa taarifa polisi au kwa wenye mamlaka.

Kulipiza kisasi ni kujiumiza mwenyewe

Vipi ikiwa haiwezekani kusuluhisha tatizo hilo kwa njia ya amani? Au namna gani ikiwa ulijaribu kufanya yote unayoweza ili kusuluhisha jambo hilo kwa njia ya amani? Usilipize kisasi. Hilo linaweza kufanya hali iwe mbaya zaidi. Usiendeleze chuki. Unaweza kujifunza kutumaini njia ya Mungu ya kusuluhisha matatizo. Biblia inasema hivi: “Mtegemee yeye, naye atatenda kwa niaba yako.”​—Zaburi 37:3-5.

Simulizi la Maisha​—ADRIÁN

Alishinda Hisia za Kulipiza Kisasi

Adrián.

Alipokuwa mvulana mdogo, Adrián alikuwa na chuki na alipigana na watu mitaani ili kulipiza kisasi. Anasema: “Mara nyingi nilipigana kwa kutumia silaha, na mara kadhaa nilikutwa mtaani nikiwa nimeumizwa vibaya karibu kufa.”

Adrián alianza kujifunza Biblia alipokuwa na umri wa miaka 16. Anasema hivi: “Nilipoendelea kujifunza Biblia, nilitambua uhitaji wa kubadili utu wangu.” Alihitaji kuondoa chuki na kuacha jeuri. Alinufaika sana na kile alichojifunza kwenye Waroma 12:17-19 kuhusu kutolipiza kisasi. Anasema: “Nilitambua kwamba Yehova atakomesha ukosefu wa haki kwa njia yake na kwa wakati wake. Hatua kwa hatua niliacha kuwa mjeuri.”

Siku moja jioni, Adrián alishambuliwa na kikundi cha wahalifu ambao zamani alipigana nao. Kiongozi wa kikundi hicho alipaaza sauti na kusema: “Jilinde!” Adrián anakiri hivi: “Nilitamani sana kulipiza kisasi.” Hata hivyo, badala ya kulipiza kisasi, alitoa sala fupi kwa Yehova na kuondoka eneo hilo.

Adrián anaendelea kusema: “Siku iliyofuata nilikutana na kiongozi wa genge hilo akiwa peke yake. Nilishikwa na hasira na nikataka kulipiza kisasi, lakini nilisali tena kimyakimya kwa Yehova anisaidie kujidhibiti. Jambo la kushangaza ni kwamba kijana huyo aliniomba msamaha kwa kusema: ‘Nisamehe kwa yaliyotokea usiku wa jana. Ukweli ni kwamba, ningependa kuwa kama wewe. Nataka kujifunza Biblia.’ Nilifurahi sana kwamba niliweza kudhibiti hasira yangu! Matokeo ni kwamba, tulianza kujifunza Biblia pamoja.”

Ili ujue mengi zaidi kuhusu simulizi la Adrián, soma gazeti la Mnara wa Mlinzi Na. 5 2016, ukurasa wa 14-15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki