-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
7 Bar-Yesu aliupinga ujumbe wa Ufalme. Njia pekee ambayo angeweza kutumia ili kudumisha cheo chake kikubwa akiwa mshauri wa Sergio Paulo ilikuwa ni kwa “kumzuia yule liwali asiwe mwamini.” (Mdo. 13:8) Hata hivyo, Sauli hakumruhusu mlozi huyo amkengeushe Sergio Paulo. Alifanya nini? Masimulizi yanasema: “Sauli, aitwaye pia Paulo, akiwa amejaa roho takatifu, akamtazama kwa makini [Bar-Yesu] na kumwambia: “Ewe mtu uliyejaa kila aina ya upunjaji na kila aina ya ulaghai, wewe mwana wa Ibilisi, wewe adui wa kila jambo la uadilifu, je, hutaacha kuzipotosha njia za Yehova zilizo sawa? Tazama! mkono wa Yehova uko juu yako, nawe utakuwa kipofu, hutaona nuru ya jua kwa kipindi fulani.” Mara moja akaangukiwa na ukungu mzito na giza, naye akazunguka akitafuta mtu wa kumshika mkono ili amwongoze.”g Matokeo? “Yule liwali alipoona jambo lililotokea, akawa mwamini kwa sababu alistaajabishwa na fundisho la Yehova.”—Mdo. 13:9-12.
-
-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
g Tangu wakati huo na kuendelea, Sauli alianza kuitwa Paulo. Watu fulani husema kwamba alijipa jina hilo la Kiroma kwa heshima ya Sergio Paulo. Hata hivyo, kwa kuwa aliendelea kuitwa Paulo hata alipoondoka Kipro, lazima kulikuwa na sababu nyingine, kwamba Paulo, “mtume wa mataifa,” aliamua kwamba tangu wakati huo na kuendelea atatumia jina lake la Kiroma. Huenda pia alitumia jina Paulo kwa sababu matamshi ya Kigiriki ya jina lake la Kiebrania, Sauli, yanafanana sana na neno la Kigiriki lenye maana mbaya.—Rom. 11:13.
-