-
Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye KuamanikaMnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
-
-
5, 6. (a) Sisi tuna mashauri gani ya hekima kwa habari ya kushughulika na wale wanaotenda dhambi nzito na hawaonyeshi toba? (Mathayo 18:17) (b) Ni maswali gani ambayo sisi tunaelekeana nayo?
5 Wakati mwanamume mmoja katika Korintho alipokuwa mkosefu wa adili kwa kutotubu, Paulo aliambia lile kundi: “Ninyi mwache kabisa kuchangamana katika ushirika pamoja na ye yote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa au mwabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyakuzi, hata msiwe mnakula pamoja na mtu huyo.” (1 Wakorintho 5:11-13, NW) Jambo ilo hilo lilipasa kutukia kwa waasi-imani, kama vile Himenayo: “Kwa habari ya binadamu anayeendeleza farakano, mkatae baada ya onyo la upole la kwanza na la pili; ukijua kwamba mtu kama huyo ameondolewa katika njia ile na anafanya dhambi.” (Tito 3:10, 11; 1 Timotheo 1:19, 20, NW) Kuepukwa kabisa kwa namna hiyo kungefaa, pia, kwa mmoja ye yote ambaye analikataa kundi: “Wao walitoka kati yetu, lakini wao hawakuwa wa aina yetu; maana kama wao wangalikuwa wa aina yetu, wangaliendelea kuwa pamoja nasi. Lakini wao walienda nje kwamba iweze kuonyeshwa wazi kwamba si wote ambao wamekuwa wa aina yetu.”—1 Yohana 2:18, 19, NW.
-
-
Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye KuamanikaMnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
-
-
Je! Amekatiliwa Nje Barabara?
7. Ni jinsi gani mwenendo wetu ungetofautiana kwa habari ya aina mbili za watenda dhambi?
7 Wakristo hawajitengi mbali na watu. Sisi tunakuwa na mawasiliano ya kikawaida pamoja na majirani, wafanya kazi wenzetu, wanashule wenzetu, na watu wengine, na tunawatolea ushuhuda hata kama watu fulani kati yao ni ‘waasherati, wenye pupa, wanyakuzi, au waabudu sanamu.’ Paulo aliandika kwamba sisi hatuwezi kuwaepuka wao kabisa, ‘ama sivyo sisi tungelazimika kwenda nje ya ulimwengu.’ Ingawa hivyo, yeye alielekeza kwamba ilipasa kuwa tofauti kwa “ndugu” aliyeishi kama hivyo: “Ninyi mwache kabisa kuchangamana katika ushirika pamoja na ye yote anayeitwa ndugu ambaye [amerudi kwenye njia kama hizo], hata msiwe mnakula pamoja na mtu huyo.”—1 Wakorintho 5:9-11; Marko 2:13-17, NW.
8. Ni shauri gani ambalo mtume Yohana aliandaa juu ya kuepuka watu?
8 Katika miandiko ya mtume Yohana, sisi tunapata shauri linalofanana na hilo ambalo linakazia jinsi Wakristo wanavyopaswa kuwaepuka kikamili watu kama hao: “Kila mmoja ambaye anajisukuma mbele na habaki katika lile fundisho la yule Kristo hana Mungu . . . Ikiwa mmoja ye yote anakuja kwa ninyi na haleti fundisho hili, msipokee kamwe huyo ndani ya nyumba zenu au kusema salamu kwake yeye. Kwa maana yeye ambaye anasema salamu [Kigiriki, khaiʹro] kwa huyo ni mshiriki katika kazi zake mbovu.”a—2 Yohana 9-11, NW.
9, 10. (a) Ni jambo gani ambalo lilitukia kwa wavunja-sheria wasiotubu katika Israeli, na kwa sababu gani? (b) Inatupasa sisi tuhisi jinsi gani juu ya mpango huo leo wa kushughulika na watu walioondoshwa nje kwa kutenda dhambi bila kutubu? (2 Petro 2:20-22)
9 Kwa sababu gani msimamo imara huo unafaa hata leo? Basi, fikiria kule kukatiliwa nje vikali ambako kuliamriwa katika Sheria ya Mungu kwa Israeli. Katika mambo mazito mbalimbali, wavunjaji sheria wa kukusudia waliuawa. (Walawi 20:10; Hesabu 15:30, 31) Jambo hilo lilipotokea, wengine, hata watu wa ukoo, hawangeweza tena kusema na yule mvunja-sheria mfu. (Walawi 19:1-4; Kumbukumbu 13:1-5; 17:1-7) Ingawa Waisraeli washikamanifu huko nyuma walikuwa wanadamu wa kikawaida wenye hisia za moyoni kama zetu, wao walijua kwamba Mungu ni mwenye haki na mwenye upendo na kwamba Sheria yake ilitoa himaya kwa usafi wao wa kiadili na wa kiroho. Kwa hiyo wao wangeweza kukubali kwamba kwa msingi mpango wake wa kukatilia nje watenda makosa ulikuwa jambo jema na lenye kufaa.—Ayubu 34:10-12.
10 Sisi tunaweza kuwa na uhakika hivyo hivyo kwamba mpango wa Mungu kwamba Wakristo wakatae kufanya ushirika pamoja na mtu fulani ambaye ameondoshwa nje kwa dhambi ya kutotubu ni himaya yenye hekima kwetu. “Iondoleeni mbali chachu ya zamani, ili ninyi mpate kuwa donge jipya, kwa kadiri ambayo ninyi mko huru bila mchachusho.” (1 Wakorintho 5:7, NW) Kwa kuepuka pia watu ambao wamejitenga na ushirika wa kundi kwa makusudi, Wakristo wanakuwa na himaya ya kutopatwa na maoni ya uchambuzi, ya kukosa uthamini, au hata ya uasi-imani.—Waebrania 12:15, 16.
Namna Gani Juu ya Watu wa Ukoo?
11, 12. (a) Ni nini lililokuwa tokeo juu ya watu wa ukoo wa Kiisraeli wakati mtenda kosa alipokatiliwa nje? (b) Toa kielezi cha manufaa za utii.
11 Kwa uhakika Mungu anatambua kwamba mara nyingi kutekeleza sheria zake za uadilifu juu ya kukatilia nje watenda makosa kunahusisha ndani watu wa ukoo na kuwaathiri. Kama ilivyotajwa juu, wakati mtenda kosa Mwisraeli alipouawa, hakuna ushirika zaidi wa kijamaa uliokuwa unawezekana. Kwa hakika, ikiwa mwana alikuwa mlevi na mlafi, wazazi wake walipaswa kumleta kwa ajili ya hukumu, na ikiwa yeye alikuwa asiyetubu, wazazi hao walipaswa kushiriki katika kule kumuua kwa haki, ‘kuondolea mbali kilicho kibaya kutoka kati ya Israeli.’ (Kumbukumbu 21:18-21, NW) Wewe unaweza kuthamini kwamba jambo hilo halingekuwa rahisi kwao. Wazia, pia, jinsi wale ndugu, dada, au babu na nyanya za mtenda kosa walivyohisi. Hata hivyo, kuweka kwao ushikamanifu kwa Mungu wao mwadilifu mbele ya shauku ya kijamaa kungeweza kuwaokolea uhai.
12 Kumbuka kile kisa cha Kora, ambaye alikuwa kiongozi katika uasi dhidi ya uongozi wa Mungu kupitia Musa. Katika haki yake kamilifu, Yehova aliona kwamba ilikuwa lazima Kora afe. Lakini washikamanifu wote walishauriwa hivi: “Nawasihi, ondokeni penye hema za hawa watu waovu, wala msiguse kitu chao cho chote, msiangamizwe katika dhambi” yao. Watu wa ukoo ambao hawakutaka kukubali onyo la Mungu walikufa pamoja na waasi hao. Lakini watu fulani wa ukoo wa Kora walichagua kwa hekima kuwa washikamanifu kwa Yehova, jambo ambalo liliokoa uhai wao na kuongoza kwenye baraka za wakati ujao.—Hesabu 16:16-33; 26:9-11; 2 Nyakati 20:19.
13. Wakristo washikamanifu wataitikia jinsi gani kama mshiriki wa jamaa ya pale pale anajitenga na ushirika?
13 Kukatilia nje kutoka kundi la Kikristo hakuhusishi ndani kifo cha mara hiyo, kwa hiyo vifungo vya kijamaa vinaendelea. Hivyo, mwanamume aliyeoa ambaye ametengwa au anajitenga na ushirika huenda bado akaishi nyumbani pamoja na mke wake Mkristo na watoto waaminifu. Staha kwa hukumu za Mungu na hatua ile ya kundi itasukuma yule mke na watoto kung’amua kwamba kwa mwendo wake, mwanamume huyo alileta mwisho wa ule ukamatano wa kiroho uliokuwa kati yao. Hata hivyo, kwa kuwa kutengwa kwake na ushirika hakukomeshi vifungo vyao vya damu au uhusiano wa ndoa, shauku na shughuli za kikawaida za jamaa zinaendelea.
14. Ni shauri gani la kimungu linalopasa kuwa na mavutano juu ya uwasiliano wetu na mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika ambaye yuko nje ya jamaa yetu ya pale pale?
14 Hali hii ni tofauti ikiwa yule ambaye ametengwa au amejitenga na ushirika ni mtu wa ukoo anayeishi nje ya jamaa ile ya pale pale, Labda ingewezekana kuzuia karibu mawasiliano yote pamoja na mtu huyo wa ukoo. Hata kama kuna mambo fulani ya kijamaa yanayotaka mawasiliano, kwa uhakika yanapasa kuwekwa katika kadiri ndogo kabisa, kupatana na ile kanuni ya kimungu: “Ninyi mwache kabisa kuchangamana katika ushirika pamoja na ye yote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa [au mwenye hatia ya dhambi nyingine nzito sana], . . . hata msiwe mnakula pamoja na mtu huyu.”—1 Wakorintho 5;11, NW.
15. Ni jinsi gani watu wa ukoo wanavyoweza kuongoza mavutano ya hisia za moyoni katika visa kama hivyo? (Zaburi 15:1-5; Marko 10:29, 30)
15 Inaeleweka kwamba huenda hilo likawa jambo gumu kwa sababu ya hisia za moyoni na vifungo vya kijamaa, kama vile upendo wa akina babu na nyanya kwa wajukuu wao. Hata hivyo. huo ni mtihani wa ushikamanifu kuelekea Mungu, kama vile ilivyotajwa na yule dada aliyenukuliwa katika ukurasa 26. Ye yote ambaye anahisi sikitiko kubwa na umizo ambalo limesababishwa hivyo na yule mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika anaweza kutiwa moyo na kielelezo kilichowekwa na watu fulani wa ukoo wa Kora.—Zaburi 84:10-12.b
-