Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Jivikeni Wenyewe Ustahimilivu’
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 1
    • “Upendo Ni Wenye Ustahimilivu”

      9. Kwa nini huenda Paulo aliwaambia Wakorintho kwamba “upendo ni wenye ustahimilivu”?

      9 Paulo alionyesha kwamba kuna uhusiano wa pekee kati ya upendo na ustahimilivu aliposema: “Upendo ni wenye ustahimilivu.” (1 Wakorintho 13:4) Msomi mmoja wa Biblia, Albert Barnes, adokeza kwamba Paulo alikazia jambo hilo kwa sababu ya ugomvi na zogo lililokuwako katika kutaniko la Kikristo huko Korintho. (1 Wakorintho 1:11, 12) Barnes asema hivi: ‘Neno lililotumiwa hapa [kumaanisha ustahimilivu] ni kinyume cha kufanya mambo haraka haraka: kusema na kuwaza kwa hasira, na kuudhika. Lamaanisha hali ya akili ya KUVUMILIA KWA MUDA MREFU unapodhulumiwa au kukasirishwa.’ Upendo na ustahimilivu unachangia sana amani ya kutaniko la Kikristo.

      10. (a) Upendo hutusaidiaje tuwe wastahimilivu, na mtume Paulo atoa shauri gani kuhusiana na habari hiyo? (b) Msomi mmoja wa Biblia alisema nini kuhusu fadhili na ustahimilivu wa Mungu? (Ona kielezi-chini.)

      10 “Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili. Upendo . . . hautafuti masilahi yao wenyewe, haupati kuwa wenye kuchokozeka.” Kwa hiyo, katika njia nyingi upendo hutusaidia tuwe wastahimilivu.a (1 Wakorintho 13:4, 5) Upendo hutuwezesha kuchukuliana kwa subira na kukumbuka kwamba sisi sote ni watu wasio wakamilifu na walio na udhaifu. Hutusaidia tuwe wenye kuwafikiria wengine na wenye kusamehe. Mtume Paulo anatutia moyo tutembee ‘tukiwa na hali kamili ya akili ya kujishusha chini na upole, tukiwa na ustahimilivu, tukichukuliana mtu na mwenzake katika upendo, tukijitahidi sana kwa bidii kushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.’—Waefeso 4:1-3.

  • ‘Jivikeni Wenyewe Ustahimilivu’
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 1
    • a Akieleza taarifa ya Paulo kwamba “upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili,” msomi wa Biblia Gordon D. Fee aandika hivi: “Katika theolojia ya Paulo sifa ya [ustahimilivu na fadhili] yaonyesha mtazamo wa Mungu kuelekea wanadamu (linganisha Rom. 2:4). Kwa upande mmoja, uvumilivu wa Mungu unaonyeshwa na jinsi anavyozuia hasira yake dhidi ya uasi wa wanadamu; kwa upande mwingine, fadhili zake zaonekana kwa jinsi anavyoonyesha sana rehema yake. Kwa hiyo ufafanuzi wa Paulo kuhusu upendo unaanza kwa ufafanuzi huu wenye maana mbili wa Mungu, ambaye kupitia Kristo ameonyesha uvumilivu na fadhili zake kuelekea wale wanaostahili kupata hukumu yake kali.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki