-
Kitabu Cha Biblia Namba 46—1 Wakorintho“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
19. Paulo atoa shauri gani ili kundi lijengwe, na mambo kupangwa kwa utaratibu?
19 “Ufuateni upendo,” Paulo aonya kwa upole. Zawadi za kiroho ni za kutumiwa kwa upendo ili kujenga kundi. Kwa sababu hiyo, kutoa unabii kwaonwa kuwa afadhali kuliko kunena kwa ndimi. Afadhali anene maneno matano yenye kueleweka ili afundishe wengine kuliko maneno elfu kumi kwa lugha isiyojulikana. Kusema ndimi mbalimbali kwafanywa ili kuwe ishara kwa wasioamini, lakini kutoa unabii ni kwa ajili ya waamini. Wao hawapaswi kuwa “watoto” katika kuelewa kwao mambo haya. Kwa habari ya wanawake, wapaswa kuwa katika ujitiisho kundini. “Mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.”—14:1, 20, 40.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 46—1 Wakorintho“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
25. Ni yapi baadhi ya mambo yenye kutokeza ya maagizo yenye mafaa yaliyomo katika Wakorintho wa Kwanza?
25 Jinsi tumepokea mafaa ya maagizo yaliyopuliziwa na Mungu kutokana na barua ya kwanza ya Paulo kwa Wakristo Wakorintho! Tafakari juu ya shauri lililotolewa juu ya migawanyiko na kufuata watu. (Sura 1-4) Kumbuka kisa cha ukosefu wa adili na jinsi Paulo alivyokazia uhitaji wa wema na usafi ndani ya kundi. (Sura 5, 6) Fikiria ushauri wake uliopuliziwa na Mungu kuhusu kutofunga ndoa, ndoa, na mtengano. (Sura 7) Fikiria mazungumzo ya mtume juu ya vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu na pia jinsi ambavyo lazima ya kujilinda na kukwaza wengine na kuangukia ibada ya sanamu ilivyotokezwa kwa mkazo. (Sura 8-10) Onyo la upole kuhusu ujitiisho unaofaa, ufikirio wa zawadi za kiroho, yale mazungumzo yenye kutumika kabisa juu ya ubora wa kuvumilia, sifa ya upendo isiyoshindwa—mambo hayo pia yamepitiwa. Na jinsi mtume alivyokazia vizuri uhitaji wa utaratibu katika mikutano ya Kikristo! (Sura 11-14) Jinsi alivyoandika chini ya upulizio wa Mungu akitetea ufufuo vizuri! (Sura 15) Yote hayo na zaidi yamepita mbele ya jicho la akili—na ni yenye thamani sana kwa Wakristo katika siku yetu!
-