-
Miaka Mia Moja ya Utawala wa Ufalme!Mnara wa Mlinzi—2015 | Novemba 15
-
-
2. Inaelekea ni watu wangapi walikuwepo Yesu alipotoa amri iliyo kwenye Mathayo 28:19 na 20? Na kwa nini tunafikia mkataa huo? (Tazama maelezo ya chini.)
2 Muda mfupi baada ya kufufuliwa, Yesu alikutana na watu zaidi ya 500, ambao baadaye wangekuwa watangazaji wa Ufalme. (1 Kor. 15:6) Inaelekea hapo ndipo Yesu aliwapa amri ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme kwa “watu wa mataifa yote,” kazi iliyokuwa kubwa sana wakati huo.a Yesu alitabiri kwamba kazi hiyo ingeendelea kufanywa mpaka “umalizio wa mfumo wa mambo,” na hivyo ndivyo ilivyo leo. Kwa hiyo, unapohubiri habari njema, unashiriki kutimiza utume na unabii huo.—Mt. 28:19, 20.
-
-
Miaka Mia Moja ya Utawala wa Ufalme!Mnara wa Mlinzi—2015 | Novemba 15
-
-
a Kuna sababu ya kuamini kwamba watu wengi waliokuwepo wakati huo walikuja kuwa Wakristo. Katika barua yake kwa Wakorintho, Paulo anawaita “ndugu zaidi ya mia tano.” Isitoshe, anaongeza hivi: “Walio wengi kati yao wapo mpaka sasa, lakini wengine wamelala usingizi katika kifo.” Hivyo, inaonekana kwamba Paulo na Wakristo wengine wa karne ya kwanza waliwajua watu wengi waliosikia moja kwa moja amri hiyo ilipotolewa.
-