-
Biblia Inasema Nini Kuhusu Useja na Ndoa?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Chagua mwenzi wa ndoa kwa hekima
Kuchagua mwenzi wa ndoa ni mojawapo ya uamuzi muhimu zaidi ambao utafanya. Soma Mathayo 19:4-6, 9, kisha mzungumzie swali hili:
Kwa nini Mkristo anapaswa kufikiria kwa makini kabla ya kufanya uamuzi wa kufunga ndoa?
Biblia inaweza kukusaidia kutambua sifa za mwenzi wa ndoa anayekufaa. Jambo muhimu zaidi, chagua mwenzi wa ndoa ambaye anampenda Yehova.b Soma 1 Wakorintho 7:39 na 2 Wakorintho 6:14. Kisha mzungumzie maswali haya:
Kwa nini Mkristo anapaswa kufunga ndoa tu na Mkristo mwenzake?
Unafikiri Yehova atahisije tukiamua kufunga ndoa na mtu ambaye hampendi Yehova?
Wanyama wawili walio tofauti sana wakifungwa nira pamoja, wataumia. Vivyo hivyo, Mkristo anayefunga ndoa na mwenzi ambaye si mwamini atapatwa na matatizo mengi
-