Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Igeni Rehema ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
    • 17. (a) Ni hali gani iliyotokea Korintho katika karne ya kwanza, naye Paulo aliwashauri wale waliokuwa katika kutaniko hilo washughulikieje hali hiyo? (b) Kwa nini onyo la upole la Paulo lilikuwa lenye kutumika, na twaweza kulitumiaje leo? (Ona sanduku pia upande wa kulia.)

      17 Ili kutusaidia tujichunguze wenyewe kuhusiana na jambo hilo, fikiria yale yaliyotokea Korintho mwaka wa 55 W.K. Huko, mwanamume fulani aliyekuwa ameondoshwa kutanikoni hatimaye alirudia maisha safi kiadili. Ndugu walipaswa kufanya nini? Je, washuku toba yake na kuendelea kumwepuka? Kinyume cha hilo, Paulo aliwasihi Wakorintho hivi: “Nyinyi mwapaswa kumsamehe kwa fadhili na kumfariji, ili kwa njia fulani mtu wa namna hiyo asipate kumezwa na huzuni yake ya kupita kiasi. Kwa hiyo, nawahimiza kwa bidii kumthibitishia upendo wenu.” (2 Wakorintho 2:7, 8) Mara nyingi, ni rahisi kwa wakosaji wenye kutubu kuona aibu au kukata tamaa. Kwa sababu hiyo, watu hao wanahitaji kuhakikishiwa kwamba wanapendwa na waamini wenzao na Yehova pia. (Yeremia 31:3; Waroma 1:12) Hilo ni muhimu. Kwa nini?

  • Igeni Rehema ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
    • 19 Kama wazee wangechukua msimamo tofauti na huo na kukataa kumsamehe mwenye kutubu, Shetani angewashinda kwa hila nyingine. Jinsi gani? Katika maana ya kwamba, angetumia vibaya hali yao ya ukali na kutokuwa na rehema. Kama mkosaji mwenye kutubu “[ali]mezwa na huzuni yake ya kupita kiasi,” au kama vile fungu hilo litafsiriwavyo katika Biblia Habari Njema, “akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa,” wazee wangekuwa na wajibu mkubwa kama nini mbele za Yehova! (Linganisha Ezekieli 34:6; Yakobo 3:1.) Baada ya kuwatahadharisha wafuasi wake dhidi ya kukwaza “mmoja wa wadogo hawa,” Yesu alisema hivi akiwa na sababu nzuri: “Kazieni uangalifu kwa nyinyi wenyewe. Ndugu yako akifanya dhambi mpe kemeo, na akitubu msamehe.”a—Luka 17:1-4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki