Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwapa Watoto Uangalifu Wanaohitaji
    Amkeni!—2005 | Februari 8
    • Kuwazoeza Watoto Bila Kuwakasirisha

      Dakt. Robert Coles, ambaye ni mwalimu na mtaalamu wa akili aliye maarufu, alisema hivi: “Mtoto anahitaji kanuni za kiadili. Ameumbwa akiwa na uhitaji huo, naye hutamani sana kuutosheleza.” Ni nani atakayetimiza uhitaji huo?

      Biblia husema hivi katika Waefeso 6:4: “Akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.” Je, unaona kwamba andiko hilo humtaka baba hasa awazoeze watoto wake kumpenda Mungu na kuheshimu viwango vyake? Katika Waefeso sura ya 6 mstari wa 1, mtume Paulo alipowaambia watoto ‘wawatii wazazi wao,’ alimaanisha wote wawili, yaani, baba na mama.a

      Bila shaka, ikiwa baba hayupo, ni lazima mama achukue daraka hilo. Mama wengi wasio na wenzi wamefanikiwa kuwalea watoto wao katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova Mungu. Hata hivyo, mama hao wakiolewa na waume Wakristo, mume ndiye anayepaswa kuchukua daraka hilo. Mama anapaswa kufuata kwa hiari mwongozo wa baba Mkristo katika kuwazoeza na kuwatia watoto nidhamu.

      Unaweza kuwazoezaje watoto wako bila ‘kuwakasirisha’? Hakuna njia moja hususa, hasa tunapotambua kwamba watoto wanatofautiana. Lakini ni lazima wazazi wafikirie kwa uzito jinsi wanavyotoa nidhamu, huku wakijitahidi kila mara kuwapenda na kuwaheshimu watoto wao. Andiko la Wakolosai 3:21 hurudia tena shauri hilo la kutowakasirisha watoto. Akina baba wanashauriwa hivi: “Msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, ili wasivunjike moyo.”

      Wazazi fulani huwapigia watoto wao kelele. Bila shaka, jambo hilo huwakasirisha watoto. Lakini Biblia hutuhimiza hivi: “Uchungu wote wenye uovu na hasira na ghadhabu na kupiga kelele na matukano na viondolewe mbali kutoka kwenu.” (Waefeso 4:31) Isitoshe, Biblia husema kwamba “mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali anahitaji kuwa mpole kwa wote.”—2 Timotheo 2:24.

  • Kuwapa Watoto Uangalifu Wanaohitaji
    Amkeni!—2005 | Februari 8
    • a Katika mstari wa kwanza, Paulo alitumia neno la Kigiriki go·neuʹsin, linalotokana na neno go·neusʹ, ambalo humaanisha “mzazi.” Lakini katika mstari wa 4 anatumia neno la Kigiriki pa·teʹres, linalomaanisha “akina baba.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki