Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 29. Ni nini kinachotimiza mfananisho wa “nyota kubwa yenye kuwaka kama taa,” na kwa nini?

      29 Sisi tumekwisha kutana na mfananisho wa nyota katika jumbe za Yesu kwa yale makundi saba, ambazo katika hizo zile nyota saba hufananisha wale wazee katika makundi.b (Ufunuo 1:20) “Nyota” zilizopakwa mafuta, pamoja na wengine wote wa wapakwa-mafuta, wanakaa katika mahali pa kimbingu katika maana ya kiroho kutoka wakati ambao wao wanatiwa muhuri kwa roho takatifu hiyo ikiwa dalili ya urithi wao wa kimbingu. (Waefeso 2:6, 7) Hata hivyo, mtume Paulo alionya kwamba kutoka miongoni mwa hao wenye mfano wa nyota wangekuja waasi-imani, wanafaraka, ambao wangeongoza kundi vibaya. (Matendo 20:29, 30) Utoaminifu kama huo ungetokeza uasi-imani mkubwa, na hao wazee walioanguka wangekuja kuwa jumuiya ya “mtu wa kuasi” ambaye angejiinua mwenyewe kwenye cheo kama cha Mungu miongoni mwa aina ya binadamu. (2 Wathesalonike 2:3, 4) Maonyo ya Paulo yalitimizwa wakati viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipotokea katika ulimwengu. Kikundi hiki kinawakilishwa vizuri na ule ufananisho wa “nyota moja kubwa ikiwaka kama taa.”

  • Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 31. (a) Ni lini viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipoanguka kutoka cheo cha “kimbingu”? (b) Maji ambayo viongozi wa kidini wanatoa yamegeukaje yakawa “pakanga,” na kukiwa na tokeo gani kwa wengi?

      31 Wakati viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipoasi Ukristo wa kweli, wao walianguka kutoka cheo kilichotukuka cha “kimbingu” kinachoelezwa na Paulo kwenye Waefeso 2:6, 7, NW. Badala ya kutoa maji safi ya ukweli, wao walitoa “pakanga,” uwongo mchungu kama vile moto wa mateso, pargatori, Utatu, na watu kuandikiwa kimbele mwisho wao; pia waliongoza mataifa kwenye vita, wakishindwa kuwajenga wawe watumishi waadilifu wa Mungu. Tokeo? Kusumishwa kiroho kwa wale walioitikadi uwongo huo. Kisa chao kilifanana na kile cha Waisraeli wasio waaminifu wa siku ya Yeremia, ambao kwao Yehova alisema: “Hapa mimi ninafanya wao kula pakanga, na mimi nitawapa maji yaliyosumishwa wanywe. Kwa kuwa kutoka manabii wa Yerusalemu uasi-imani umetoka na kwenda kwenye bara lote.”—Yeremia 9:15; 23:15, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki