Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ukombozi Unaolingana Kwa Ajili Ya Wote
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Februari 15
    • Ukombozi Unaolingana

      10. Kwa nini dhabihu za wanyama hazingeweza kufunika dhambi za ainabinadamu vya kutosha?

      10 Yaliyotangulia yanaonyesha kwamba ni lazima ukombozi uwe sawasawa kabisa na kile ambacho huo uko badala yacho, au ambacho unafunika. Dhabihu za wanyama zilizotolewa na wanaume waaminifu kutoka Habili na kuendelea hazingeweza kwa kweli kufunika dhambi za wanadamu, kwa kuwa wanadamu wana ubora zaidi kuliko hayawani wasioweza kusababu. (Zaburi 8:4-8) Kwa hivyo Paulo angeweza kuandika kwamba “haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.” Dhabihu hizo zingetumika tu kama funiko lililo picha, au mfano wa kutazamia ule ukombozi ambao ungekuja.—Waebrania 10:1-4.

      11, 12. (a) Kwa nini maelfu ya mamilioni ya binadamu hawakupaswa kufa vifo vya kidhabihu ili kufunika hali ya dhambi ya ainabinadamu? (b) Nani tu angeweza kutumika akiwa “ukombozi unaolingana,” na kifo chake ni cha kusudi gani?

      11 Ukombozi huu ulioonyeshwa kimbele ulipaswa kuwa ulinganisho ulio sawasawa kabisa na Adamu, kwa kuwa adhabu ya kifo ambayo Mungu aliwekea Adamu kihaki ilitokeza kulaaniwa kwa jamii ya kibinadamu. “Katika Adamu wote wanakufa,” chasema 1 Wakorintho 15:22. Kwa hivyo haikuwa lazima kabisa maelfu ya mamilioni ya wanadamu mmoja mmoja wafe vifo vya dhabihu ili kulingana na kila mtu wa mzao wa Adamu. “Kwa mtu mmoja [Adamu] dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti.” (Warumi 5:12) Na “kwa kuwa mauti ililetwa na mtu,” fidia kwa ainabinadamu ingeweza pia ‘kuletwa na mtu.’—1 Wakorintho 15:21.

      12 Mtu ambaye angeweza kuwa ukombozi angetakiwa awe binadamu mkamilifu wa mnofu na damu—aliye sawa kabisa na Adamu. (Warumi 5:14) Kiumbe cha kiroho au “Mungu-Binadamu” hangeweza kusawazisha mizani ya haki. Ni binadamu mkamilifu tu, mtu asiyekuwa chini ya hukumu ya kifo ya Kiadamu, ambaye angeweza kutoa “ukombozi unaolingana,” mmoja unaolingana kikamilifu na Adamu. (1 Timotheo 2:6, NW)a Kwa kudhabihu uhai wake kwa hiari, “Adamu wa mwisho” angeweza kulipa mshahara kwa ajili ya dhambi ya “Mtu wa kwanza, Adamu.”—1 Wakorintho 15:45; Warumi 6:23.

  • Ukombozi Unaolingana Kwa Ajili Ya Wote
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Februari 15
    • a Neno la Kigiriki linalotumiwa hapa, an.tiʹly.tron, halitokei mahali pengine popote katika Biblia. Lina uhusiano na neno ambalo Yesu alitumia kwa ukombozi (lyʹtron) katika Marko 10:45. Hata hivyo, The New International Dictionary of New Testament Theology inaonyesha kwamba an.tiʹly.tron ‘linakazia wazo la kubadilisha.’ Kwa kufaa, New World Translation inalitafsiri “ukombozi unaolingana.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki