-
Imarisha Imani Yako Kuhusu Mambo UnayotumainiMnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Oktoba
-
-
2 Kwa upande mwingine, watu wengi katika ulimwengu wa Shetani wana aina fulani ya tumaini, lakini wana mashaka ikiwa kwa kweli matumaini yao yatawahi kutimia. Kwa mfano, wacheza kamari wengi wanatumaini kwamba siku moja watashinda kiasi kikubwa cha pesa, lakini hawana uhakika kuhusu jambo hilo. Tofauti na hilo, imani ya kweli ni “tarajio lililohakikishwa” la tumaini letu la Kikristo. (Ebr. 11:1) Hata hivyo, huenda ukajiuliza, ‘Ninawezaje kuwa na uhakika hata zaidi kwamba tarajio langu litatimizwa? Kuna manufaa gani ya kuwa na imani yenye nguvu kuhusu mambo ninayotumaini?’
3. Imani ya kweli ya Kikristo inategemea nini?
3 Imani si sifa ambayo wanadamu wasio wakamilifu huzaliwa nayo, wala haijitokezi tu. Imani ya Kikristo hutokezwa roho takatifu ya Mungu inapofanya kazi ndani ya moyo wa mtu aliye tayari kuiruhusu ifanye kazi ndani yake. (Gal. 5:22) Biblia haisemi kwamba Yehova ana imani au ikiwa anahitaji imani. Kwa kuwa Yehova ni mweza yote na mwenye hekima yote, hakuna kitu kinachoweza kumzuia asitimize kusudi lake. Baba yetu wa mbinguni ana uhakika kabisa kwamba baraka alizoahidi zitatimia, na kwake ni kama tayari zimetimia. Kwa hiyo, anasema, “Yamekuwa!” (Soma Ufunuo 21:3-6.) Imani ya Kikristo inategemea uhakika wa kwamba Yehova ni “Mungu mwaminifu,” ambaye sikuzote hutimiza kile anachoahidi.—Kum. 7:9.
KUJIFUNZA KUTOKANA NA IMANI YA WATUMISHI WA ZAMANI WA MUNGU
4. Watumishi wa Mungu walioishi zamani walikuwa na tumaini gani lenye thamani?
4 Sura ya 11 ya kitabu cha Waebrania ina orodha ya majina 16 ya wanaume na wanawake wenye imani. Mwandikaji wa kitabu hicho aliongozwa na roho ya Mungu kuandika kuhusu wanaume na wanawake hao na pia watumishi wengine wengi “[waliotolewa] ushahidi kupitia imani yao.” (Ebr. 11:39) Wote walikuwa na “tarajio lililohakikishwa” kwamba Mungu angetokeza “uzao” ulioahidiwa ili uponde uasi wa Shetani na kutimiza kusudi la awali la Yehova. (Mwa. 3:15) Watumishi hao waaminifu walikufa kabla ya “uzao” ulioahidiwa, yaani, Yesu Kristo, kufungua njia ya wanadamu kuishi mbinguni. (Gal. 3:16) Hata hivyo, tunajua kwamba watafufuliwa wapate uhai mkamilifu kwenye dunia paradiso kwa sababu ahadi za Yehova lazima zitimie!—Zab. 37:11; Isa. 26:19; Hos. 13:14.
-
-
Imarisha Imani Yako Kuhusu Mambo UnayotumainiMnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Oktoba
-
-
7. Kwa fadhili Yehova ametupatia maandalizi gani ili tusitawishe imani yenye nguvu, na tunapaswa kutumiaje maandalizi hayo?
7 Kwa fadhili, Yehova ametupatia Neno lake Biblia ili tudumishe imani yenye nguvu. Ili tuwe wenye “furaha” na ‘tufanikiwe,’ tunapaswa kusoma Neno la Mungu kwa ukawaida, ikiwezekana kila siku. (Zab. 1:1-3; soma Matendo 17:11.) Kisha, kama watumishi wa zamani wa Yehova, tunapaswa kuendelea kutafakari ahadi za Mungu na kutii maagizo yake. Pia, Yehova ametubariki kwa kutuandalia chakula kingi cha kiroho kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Tukithamini maandalizi ya kiroho ambayo Yehova ametupatia, tutakuwa kama watumishi wake wa zamani wenye imani ambao walikuwa na “tarajio lililohakikishwa” katika tumaini lao la Ufalme.
-