Waebrania
10 Kwa kuwa Sheria ina kivuli+ cha mambo mema yatakayokuja, lakini si umbo halisi la mambo hayo, watu hawawezi kamwe kuwafanya wale wanaokaribia kuwa wakamilifu+ kwa dhabihu zilezile mwaka baada ya mwaka ambazo wao huendelea kuzitoa. 2 Kama sivyo, je, dhabihu hazingekoma kutolewa, kwa sababu wale wanaotoa utumishi mtakatifu ambao walikuwa wamesafishwa mara moja kwa wakati wote hawangekuwa na ufahamu wa dhambi tena?+ 3 Kinyume cha hilo, kwa dhabihu hizo kuna kukumbusha juu ya dhambi mwaka baada ya mwaka,+ 4 kwa maana haiwezekani damu ya ng’ombe na ya mbuzi kuondolea mbali dhambi.+
5 Kwa hiyo wakati yeye anapokuja katika ulimwengu anasema: “ ‘Dhabihu na toleo wewe hukutaka,+ bali ulinitayarishia mwili.+ 6 Hukukubali matoleo mazima ya kuteketezwa na toleo la dhambi.’+ 7 Ndipo nikasema, ‘Tazama! Nimekuja (katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu)+ ili kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.’ ”+ 8 Baada ya kwanza kusema: “Hukutaka wala hukukubali dhabihu na matoleo na matoleo mazima ya kuteketezwa na toleo la dhambi”+—dhabihu zinazotolewa kulingana na Sheria+— 9 ndipo anasema: “Tazama! nimekuja kufanya mapenzi yako.”+ Anaondolea mbali lile la kwanza ili asimamishe lile la pili.+ 10 Kwa hayo “mapenzi”+ yaliyosemwa sisi tumetakaswa+ kupitia toleo+ la mwili wa Yesu Kristo+ mara moja kwa wakati wote.
11 Pia, kila kuhani husimama mahali pake+ siku baada ya siku+ ili kutoa utumishi wa watu wote na kutoa dhabihu zilezile mara nyingi, kwa kuwa hizo haziwezi kamwe kuondoa kabisa dhambi.+ 12 Lakini mtu huyu alitoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi daima+ na kuketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu,+ 13 tangu wakati huo na kuendelea akingojea mpaka adui zake wawekwe kuwa kiti cha miguu yake.+ 14 Kwa maana ni kwa toleo moja la dhabihu+ kwamba yeye amewafanya wale wanaotakaswa wawe wakamilifu+ daima. 15 Zaidi ya hayo, roho takatifu+ pia inatutolea ushahidi, kwa maana baada ya kusema: 16 “ ‘Hili ndilo agano nitakalofanya kwao baada ya siku hizo,’ asema Yehova. ‘Nitazitia sheria zangu katika mioyo yao, nami nitaziandika katika akili zao,’ ”+ 17 inasema baadaye: “Nami sitazikumbuka tena dhambi zao hata kidogo na matendo yao ya kuasi sheria.”+ 18 Sasa mahali palipo na msamaha+ wa mambo hayo, hapana tena toleo kwa ajili ya dhambi.+
19 Kwa hiyo, akina ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa njia ya kuingia+ katika mahali patakatifu+ kwa damu ya Yesu, 20 aliyotuzindulia kuwa njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia,+ yaani, mwili wake,+ 21 na kwa kuwa tuna kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu,+ 22 acheni tukaribie tukiwa na mioyo ya kweli katika uhakikisho kamili wa imani, mioyo yetu ikiisha kunyunyizwa kutokana na dhamiri+ ya uovu na miili yetu kuoshwa kwa maji safi.+ 23 Acheni tushike imara tangazo la hadharani la tumaini+ letu bila kuyumba-yumba,+ kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.+ 24 Na acheni tufikiriane ili kuchocheana+ katika upendo na matendo mazuri,+ 25 bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe,+ kama vile wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo,+ na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri mnavyoona siku ile kuwa inakaribia.+
26 Kwa maana tukizoea kutenda dhambi kimakusudi+ baada ya kupokea ujuzi sahihi juu ya kweli,+ hakuna tena dhabihu yoyote iliyobaki kwa ajili ya dhambi,+ 27 lakini kuna tarajio hakika lenye kuogopesha la hukumu+ na kuna wivu unaowaka moto ambao utawateketeza wale wanaopinga.+ 28 Mtu yeyote ambaye ameipuuza sheria ya Musa hufa bila huruma, kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu.+ 29 Je, mnafikiri atahesabiwa kuwa anastahili adhabu kali zaidi namna gani,+ mtu ambaye amemkanyagia chini+ Mwana wa Mungu na ambaye ameiona kuwa yenye thamani ya kawaida tu damu+ ya agano ambayo kupitia hiyo alitakaswa, na ambaye ameitendea kwa dharau ile roho+ ya fadhili zisizostahiliwa? 30 Kwa maana tunamjua yeye aliyesema: “Kisasi ni changu; mimi nitalipa”;+ na tena: “Yehova atawahukumu watu wake.”+ 31 Ni jambo lenye kuogopesha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.+
32 Hata hivyo, endeleeni kuzikumbuka zile siku za zamani ambazo, baada ya kutiwa nuru,+ mlivumilia shindano kubwa chini ya mateso,+ 33 nyakati fulani mkifunuliwa wazi kama katika jumba la maonyesho+ kwenye shutuma na dhiki pia, na nyakati fulani mlipokuwa washiriki pamoja na wale waliokuwa wakipatwa na jambo la namna hiyo.+ 34 Kwa maana mliwasikitikia wale waliokuwa gerezani na pia kwa shangwe mkavumilia kuporwa+ mali zenu, mkijua ninyi wenyewe mna miliki bora na yenye kudumu.+
35 Kwa hiyo, msiutupilie mbali uhuru wenu wa kusema,+ ulio na thawabu+ kubwa ya kulipwa. 36 Kwa maana mnahitaji kuwa na uvumilivu,+ ili kwamba, baada ya kufanya mapenzi ya Mungu,+ mpokee utimizo wa ile ahadi.+ 37 Kwa maana bado “muda kidogo sana,”+ na “yeye anayekuja atafika naye hatakawia.”+ 38 “Lakini mwadilifu wangu ataishi kwa sababu ya imani,”+ na, “akirudi nyuma kwa kutetemeka, nafsi yangu haipendezwi naye.”+ 39 Sasa sisi si namna ya watu wanaorudi nyuma kwenye maangamizi,+ bali sisi ni namna ya watu walio na imani ya kuihifadhi hai nafsi.+