Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 12/1 kur. 29-31
  • “Kumbukeni Siku Zilizopita” kwa Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kumbukeni Siku Zilizopita” kwa Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hamasa na Kitia-moyo
  • Kujifunza Kutokana na Makosa ya Wakati Uliopita
  • Kiasi na Shukrani
  • Hupaswi Kumsahau Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kitabu Cha Biblia Namba 5—Kumbukumbu La Torati
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Unaweza Kuboresha Kumbukumbu Yako
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Usife Moyo Katika Shindano la Mbio la Kupata Uhai!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 12/1 kur. 29-31

“Kumbukeni Siku Zilizopita” kwa Nini?

“KUMBUKENI siku zilizopita.” Onyo hilo la upole la mtume Paulo, lililoandikwa wapata mwaka wa 61 W.K., lilielekezewa Wakristo Waebrania katika Yudea. (Waebrania 10:32, The New English Bible) Ni nini kilichosababisha maneno hayo? Kwa nini kulikuwa na uhitaji kwa waabudu hao wa Yehova wa karne ya kwanza kutosahau wakati uliopita? Je, twaweza kunufaika kwa kutii kikumbusha kama hicho leo?

Kwa karne nyingi, waandikaji wa Biblia wameonya tena na tena dhidi ya kupuuza au kutokuwa waangalifu kuhusu wakati uliopita. Nyakati na matukio ya zamani yalipaswa kukumbukwa na kufikiriwa. Hata Yehova alisema hivi: “Kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi.” (Isaya 46:9) Acheni tuchunguze sababu tatu zenye nguvu za kulitii onyo hilo la upole.

Hamasa na Kitia-moyo

Kwanza, kwaweza kuwa chanzo kikubwa cha hamasa na kitia-moyo. Paulo alipoandika barua yake kwa kutaniko la Waebrania, alikuwa akiandikia Wakristo wenzake ambao imani yao ilitahiniwa kila siku kwa sababu ya upinzani kutoka kwa Wayahudi. Kwa kutambua uhitaji wao wa kukuza uvumilivu, Paulo alisema hivi: “Lakini zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu.” (Waebrania 10:32) Kukumbuka kwao matendo ya wakati uliopita ya uaminifu-mshikamanifu katika vita ya kiroho kungewapa moyo mkuu uliohitajiwa ili kumaliza shindano la mbio. Vivyo hivyo, nabii Isaya aliandika hivi: “Kumbukeni haya, mkajionyeshe kuwa waume.” (Isaya 46:8) Yesu Kristo aliliambia hivi kutaniko la Efeso akifikiria tokeo kama hilo lenye kutamanika: “Kumbuka ni wapi ulikoanguka [upendo uliokuwa nao mwanzoni]; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza.”—Ufunuo 2:4, 5.

Lile himizo la bidii la “kumbuka siku za kale, [ku]tafakari miaka ya vizazi vingi” lilikuwa habari yenye kutokea tena na tena katika hotuba ambazo Musa aliwatolea Waisraeli, alipolisihi sana hilo taifa lionyeshe uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova bila hofu. (Kumbukumbu la Torati 32:7) Ona maneno yake, yaliyorekodiwa kwenye Kumbukumbu la Torati 7:18: “Usiwaogope [Wakanaani]; kumbuka sana BWANA, Mungu wako, alivyomfanya Farao na Misri yote.” Kule kukumbuka matendo yenye kuokoa ya Yehova kwa niaba ya watu wake kulipaswa kuwa kichocheo cha kuendelea kwao kushikamana kwa uaminifu na sheria za Mungu.—Kumbukumbu la Torati 5:15; 15:15.

Kwa kuhuzunisha, mara nyingi Waisraeli walishindwa na dhambi ya usahaulifu. Tokeo likiwa nini? “Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu, wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli. Hawakuukumbuka mkono wake, wala siku ile alipowakomboa na mtesi.” (Zaburi 78:41, 42) Hatimaye, usahaulifu wao wa amri za Yehova ulisababisha kukataliwa kwao naye.—Mathayo 21:42, 43.

Kielelezo chema kiliwekwa na mtungazaburi aliyeandika hivi: “Nitayakumbuka matendo ya BWANA; naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale. Pia nitaitafakari kazi yako yote; nitaziwaza habari za matendo yako.” (Zaburi 77:11, 12) Kukumbuka huko kwa njia ya kutafakari juu ya utumishi mwaminifu-mshikamanifu wa wakati uliopita na matendo yenye upendo ya Yehova kutatuandalia hamasa, kitia-moyo, na uthamini unaohitajiwa. Pia, “kukumbuka siku za hapo zamani” kwaweza kuondolea mbali uchovu na kwaweza kutuchochea tufanye yote tuwezayo kudumisha uvumilivu mwaminifu.

Kujifunza Kutokana na Makosa ya Wakati Uliopita

Pili, kutosahau kwaweza kuwa njia ya kujifunza kutokana na makosa ya wakati uliopita na matokeo yayo. Akifikiria hilo, Musa alishauri Waisraeli hivi: “Kumbuka, usisahau ulivyomtia BWANA, Mungu wako, kasirani jangwani; tangu siku uliyotoka nchi ya Misri hata mlipofika mahali hapa, mmekuwa na uasi juu ya BWANA.” (Kumbukumbu la Torati 9:7) Kama Musa alivyoonyesha, tokeo la kutotii huko kwa Waisraeli lilikuwa kwamba ‘BWANA Mungu wao aliwaongoza miaka arobaini katika jangwa.’ Kwa nini walitiwa moyo kukumbuka hilo? Ilikuwa ili wanyenyekezwe na wasahihishe njia zao za uasi ili kwamba ‘wangezishika amri za BWANA, Mungu wao, wapate kwenda katika njia zake na kumcha.’ (Kumbukumbu la Torati 8:2-6) Walipaswa kujifunza katika maana ya kutorudia makosa yao ya wakati uliopita.

Mwandikaji mmoja alionelea hivi: “Mtu mwenye busara hufaidika kutokana na mambo ya kibinafsi yaliyompata, bali mtu mwenye hekima hufaidika kutokana na mambo yaliyowapata wengine.” Ingawa Musa aliwasihi watu wa Israeli wanufaike kwa kufikiria makosa yao wenyewe ya zamani, mtume Paulo aliwaonya wengine kwa upole—kutaniko la Korintho la karne ya kwanza na, kwa upana zaidi, sisi—tufyonze somo kutokana na rekodi hiyohiyo ya kihistoria. Aliandika hivi: ‘Basi mambo hayo yaliwapata wao [Waisraeli] kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.’ (1 Wakorintho 10:11) Yesu Kristo alikuwa akifikiria tukio jingine la kale la Kibiblia na ule uhitaji wa kujifunza kutokana nalo aliposema hivi: “Mkumbukeni mkewe Lutu.” (Luka 17:32; Mwanzo 19:1-26) Samuel Taylor Coleridge, mshairi na mwanafalsafa Mwingereza aliandika hivi: “Ikiwa watu wangeweza kujifunza kutokana na historia, ni masomo yaliyoje iwezayo kutufundisha!”

Kiasi na Shukrani

Tatu, kukumbuka kwaweza kutokeza ndani yetu zile sifa zenye kumpendeza Mungu za kiasi na shukrani. Tushangiliapo katika vipengele mbalimbali vya paradiso yetu ya kiroho ya ulimwenguni pote, na tusisahau kamwe kuwa hiyo hukalia mawe fulani ya kujengea. Hayo hutia ndani uaminifu-mshikamanifu, upendo, kujidhabihu, ujasiri kunapokuwa na taabu, uvumilivu, ustahimilivu, na imani—sifa zinazoonyeshwa na ndugu na dada zetu Wakristo ambao miongo kadhaa iliyopita walianzisha kazi katika nchi mbalimbali. Kikimalizia ripoti yacho juu ya historia ya siku ya kisasa ya watu wa Mungu katika Mexico, Kitabu-Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 1995 (cha Kiingereza) kilisema hivi: “Kwa watu ambao wameshirikiana na Mashahidi wa Yehova karibuni tu, majaribu yaliyokabiliwa na wale walioshiriki katika kuifungua kazi Mexico yaweza kuwashangaza. Wao wamezoea paradiso ya kiroho ambamo mna wingi wa chakula cha kiroho, ambamo mna mamia ya maelfu ya washiriki wanaomhofu Mungu, na ambamo utumishi kwa Mungu unatolewa katika njia iliyopangwa vizuri.”

Mara nyingi hao waliofungua kazi mahali papya walihubiri wakiwa peke yao au katika vikundi vidogo vilivyo peke yavyo. Walikabili upweke, uhitaji, na mitihani mingine mikali ya uaminifu-maadili walipokuwa wakistahimili katika kupiga mbiu ya ujumbe wa Ufalme. Ingawa wengi wa watumishi hao wa nyakati za zamani wamekufa, yachangamsha moyo kama nini kujua kwamba Yehova anakumbuka utumishi wao mwaminifu! Mtume Paulo alihakikisha hilo alipoandika hivi: “Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake.” (Waebrania 6:10) Ikiwa Yehova hukumbuka kwa uthamini, je, sisi hatupaswi kufanya vivyo hivyo katika roho ya shukrani?

Wale ambao ni wapya katika kweli waweza kupata habari hiyo ya kihistoria kupitia kichapo Jehovah’s Witnesses—Proclaimers of God’s Kingdom.a Zaidi, ikiwa tuna pendeleo la kuwa katika familia au katika kutaniko la Kikristo ambalo washiriki walo wanatia ndani ndugu au dada wenye umri mkubwa zaidi ambao wametumikia kwa muda mrefu, twasihiwa sana katika roho ya Kumbukumbu la Torati 32:7 “kumbuka siku za kale, tafakari miaka ya vizazi vingi; mwulize baba yako, naye atakuonyesha; wazee wako, nao watakuambia.”

Ndiyo, kukumbuka matendo ya zamani ya ujitoaji-kimungu kwaweza kutuchochea tuendelee kuvumilia kwa shangwe katika utumishi wetu wa Kikristo. Pia, historia ina masomo tunayohitaji kujifunza. Na kutafakari juu ya paradiso yetu ya kiroho yenye baraka za Mungu hutokeza ndani yetu sifa zenye kupendeza za kiasi na shukrani. Kwa kweli, “kumbukeni siku zilizopita.”

[Maelezo ya Chini]

a Kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki