Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 10/22 uku. 31
  • Ni Nini Huwafanya Watu Wawe Wenye Furaha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Huwafanya Watu Wawe Wenye Furaha?
  • Amkeni!—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Jinsi ya Kupata Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Furaha ya Kweli Katika Kumtumikia Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Jitihada ya Kutafuta Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 10/22 uku. 31

Ni Nini Huwafanya Watu Wawe Wenye Furaha?

Kwa miongo miwili kikundi cha watafiti ulimwenguni pote wamekuwa wakifanya uchunguzi kwa njia yenye utaratibu juu ya furaha. Matokeo ya uchunguzi wao yalikuwa nini? “Furaha haionekani kutegemea sana hali za nje,” laripoti gazeti Scientific American.

Jarida hili la kisayansi pia lilisema hivi: “Kuwa na mali hakumaanishi kuwa na furaha. Watu hawajawa wenye furaha zaidi tamaduni zao zilipokuwa tajiri zaidi. . . . Katika mataifa mengi uhusiano kati ya mapato na furaha ni mdogo sana.”

Uchunguzi huo mbalimbali ulionyesha tabia nne ambazo huwatambulisha watu wenye furaha: Wao hujipenda na kujiheshimu sana, wahisi kwamba wanadhibiti maisha yao wenyewe, wao hutazamia mazuri, nao ni wacheshi. Kwa kuongezea, ndoa nzuri na mahusiano ya kibinafsi ya karibu ni mambo yanayochangia maisha yenye furaha, na mambo haya yaelekea kuongeza afya na maisha marefu zaidi.

Inapendeza kwamba Scientific American liliripoti: “Watu walio watendaji katika dini pia wameripotiwa kuwa na furaha. Uchunguzi mmoja wa Gallup ulionyesha kwamba watu wa kidini sana walikuwa na uwezekano wa mara mbili zaidi kuliko wale wenye kujifungamanisha kidogo na dini katika kujitangaza kuwa wenye furaha sana. Uchunguzi mwingine mbalimbali, kutia ndani ushirikiano wa mataifa 16 katika uchunguzi wa watu 166,000 katika mataifa 14, umeonyesha kwamba furaha na maisha yenye uradhi huongezeka wakati watu wanapokuwa na uhusiano wenye nguvu wa kidini na kuhudhuria ibada mara nyingi.”

Zamani sana mtunga-zaburi Daudi alifunua kwamba furaha ya kibinafsi inahusiana kwa ukaribu sana na ibada yenye muungano ya Yehova Mungu, akiandika: “Nalifurahi waliponiambia, na twende nyumbani kwa BWANA.”—Zaburi 122:1.

Si ajabu kwamba mtume Paulo aliwasihi sana Wakristo wenzi: “Acheni tufikiriane ili kuchocheana kwenye upendo na kazi zilizo bora, si kuachilia mbali kukusanyika pamoja sisi wenyewe”! (Waebrania 10:24, 25) Kwa kweli, kukusanyika ili kumwabudu Mungu pamoja na wale wenye imani yenye thamani kama yetu ni tukio lenye shangwe kwa wapendao kweli ya Biblia. Mamilioni ya Mashahidi wa Yehova wamegundua hili kuwa kweli nao wakualika ujionee mwenyewe kwa kuungana nao katika ibada kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu nawe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki