Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mfikirieni Sana Yeye Ambaye Amevumilia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • ‘Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu’

      20, 21. Yehova anatutazamia tufanye nini kuhusiana na uvumilivu, na azimio letu linapaswa kuwa nini?

      20 Yesu alijua kwamba haingekuwa rahisi kuwa mfuasi wake, na kwamba uvumilivu ungehitajiwa. (Yohana 15:20) Alikuwa tayari kuweka mfano, akijua kwamba mfano wake ungewatia wengine nguvu. (Yohana 16:33) Ni kweli kwamba Yesu aliweka kielelezo kikamilifu cha uvumilivu, lakini sisi si wakamilifu. Yehova anatazamia tufanye nini? Petro anaeleza: “Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi kielelezo ili mfuate hatua zake kwa ukaribu.” (1 Petro 2:21) Yesu alituwekea “kielelezo,” au mfano wa kufuata, tunapokuwa katika majaribu.a Uvumilivu wake chini ya hali tofauti-tofauti unaweza kulinganishwa na “hatua,” au nyayo. Hatuwezi kufuata hatua hizo kikamilifu, lakini tunaweza kuzifuata “kwa ukaribu.”

  • “Mfikirieni Sana Yeye Ambaye Amevumilia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • a Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “kielelezo,” linamaanisha “kuandika chini ya maandishi.” Mtume Petro ndiye mwandikaji pekee wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo aliyetumia neno hilo ambalo inasemwa kwamba linamaanisha “‘maandishi ya kuiga’ yaliyoandikwa ifaavyo katika kitabu cha kuandikia cha mtoto, ili mtoto afuatishe kwa kadiri awezavyo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki