-
Mwapaswa Kuwa Watu wa Namna Gani?Huduma ya Ufalme—1995 | Agosti
-
-
1 Siku ya kutozwa hesabu yakaribia kwa wanadamu wote. Biblia huiita “siku ya Yehova.” Ni wakati ambapo hukumu ya kimungu itatekelezwa dhidi ya waovu; pia ni wakati wa ukombozi kwa waadilifu. Watu wote walio hai wakati huo watatozwa hesabu ya jinsi walivyoishi maisha yao. Akiwa na hilo akilini, Petro atokeza swali hili lenye kuchunguza: “Mwapaswa kuwa watu wa namna gani”? Yeye akazia umaana wa ‘matendo matakatifu ya mwenendo, vitendo vya ujitoaji kimungu, na kuiweka akilini siku ya Yehova,’ na vilevile uhitaji wa kuwa ‘bila doa, bila waa, na katika amani.’—2 Pet. 3:11-14, NW.
-
-
Mwapaswa Kuwa Watu wa Namna Gani?Huduma ya Ufalme—1995 | Agosti
-
-
4 Kuendelea “kukumbuka” siku ya Yehova kwamaanisha kuiweka mbele ya mawazo yetu ya kila siku, bila kuiondoa kamwe akilini na kuitupilia mbali iwe isiyo ya maana sana. Humaanisha kuweka masilahi ya Ufalme kwanza maishani mwetu.—Mt. 6:33.
-