-
Mwapaswa Kuwa Watu wa Namna Gani?Huduma ya Ufalme—1995 | Agosti
-
-
1 Siku ya kutozwa hesabu yakaribia kwa wanadamu wote. Biblia huiita “siku ya Yehova.” Ni wakati ambapo hukumu ya kimungu itatekelezwa dhidi ya waovu; pia ni wakati wa ukombozi kwa waadilifu. Watu wote walio hai wakati huo watatozwa hesabu ya jinsi walivyoishi maisha yao. Akiwa na hilo akilini, Petro atokeza swali hili lenye kuchunguza: “Mwapaswa kuwa watu wa namna gani”? Yeye akazia umaana wa ‘matendo matakatifu ya mwenendo, vitendo vya ujitoaji kimungu, na kuiweka akilini siku ya Yehova,’ na vilevile uhitaji wa kuwa ‘bila doa, bila waa, na katika amani.’—2 Pet. 3:11-14, NW.
-
-
Mwapaswa Kuwa Watu wa Namna Gani?Huduma ya Ufalme—1995 | Agosti
-
-
5 Bila Doa, Bila Waa, na Katika Amani: Tukiwa sehemu ya umati mkubwa, ‘tumefua mavazi yetu, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.’ (Ufu. 7:14) Basi kuwa bila “doa” humaanisha, kwamba ni lazima kwa uimara tulinde maisha yetu yaliyo safi na wakfu dhidi ya kuchafuliwa na vitu visivyo safi vya ulimwengu. Twajiweka wenyewe tukiwa “bila waa” kwa kukataa kuruhusu ufuatiaji wa vitu vya kimwili visivyo vya kimungu uharibu utu wetu wa Kikristo. (Yak. 1:27; 1 Yoh. 2:15-17) Twaonyesha kwamba twaishi “katika amani” kwa kuonyesha “amani ya Mungu” katika kushughulika kwetu pamoja na wengine.—Flp. 4:7; Rum. 12:18; 14:19.
-