Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Aharibu Kiburi cha Tiro
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 32. Yohana alitoa onyo gani, nasi twaweza kulitumiaje?

      32 Haidhuru hali yetu ya kiuchumi, Ufalme wapaswa kutangulizwa nyakati zote maishani mwetu. Ni muhimu kwamba tusiyasahau kamwe maneno ya mtume Yohana: “Msiwe mkipenda ama ulimwengu ama vitu vilivyo katika ulimwengu. Ikiwa yeyote aupenda ulimwengu, kumpenda Baba hakumo katika yeye.” (1 Yohana 2:15) Ni kweli kwamba twalazimika kutumia mipango ya kiuchumi ya ulimwengu ili kujiruzuku. (2 Wathesalonike 3:10) Basi, ‘twautumia ulimwengu’—lakini hatuutumii “kwa ukamili.” (1 Wakorintho 7:31) Ikiwa twavipenda mno vitu vya kimwili—vitu vilivyo ulimwenguni—hatumpendi tena Yehova. Kufuatia “tamaa ya mwili na tamaa ya macho na wonyesho wa mtu wa kujivunia njia yake ya kutegemeza maisha” hakupatani na kufanya mapenzi ya Mungu.d Na kufanya mapenzi ya Mungu ndiko kuongozapo kwenye uhai wa milele.—1 Yohana 2:16, 17.

  • Yehova Aharibu Kiburi cha Tiro
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • d “Wonyesho . . . wa kujivunia” ni usemi uliotumiwa kutafsiri neno la Kigiriki a·la·zo·niʹa, linalofafanuliwa kuwa “maoni yasiyo na heshima na ya bure tu yanayomfanya mtu aweke tumaini katika uthabiti wa vitu vya duniani.”—The New Thayer’s Greek-English Lexicon.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki