-
Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye KuamanikaMnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
-
-
8. Ni shauri gani ambalo mtume Yohana aliandaa juu ya kuepuka watu?
8 Katika miandiko ya mtume Yohana, sisi tunapata shauri linalofanana na hilo ambalo linakazia jinsi Wakristo wanavyopaswa kuwaepuka kikamili watu kama hao: “Kila mmoja ambaye anajisukuma mbele na habaki katika lile fundisho la yule Kristo hana Mungu . . . Ikiwa mmoja ye yote anakuja kwa ninyi na haleti fundisho hili, msipokee kamwe huyo ndani ya nyumba zenu au kusema salamu kwake yeye. Kwa maana yeye ambaye anasema salamu [Kigiriki, khaiʹro] kwa huyo ni mshiriki katika kazi zake mbovu.”a—2 Yohana 9-11, NW.
9, 10. (a) Ni jambo gani ambalo lilitukia kwa wavunja-sheria wasiotubu katika Israeli, na kwa sababu gani? (b) Inatupasa sisi tuhisi jinsi gani juu ya mpango huo leo wa kushughulika na watu walioondoshwa nje kwa kutenda dhambi bila kutubu? (2 Petro 2:20-22)
9 Kwa sababu gani msimamo imara huo unafaa hata leo? Basi, fikiria kule kukatiliwa nje vikali ambako kuliamriwa katika Sheria ya Mungu kwa Israeli. Katika mambo mazito mbalimbali, wavunjaji sheria wa kukusudia waliuawa. (Walawi 20:10; Hesabu 15:30, 31) Jambo hilo lilipotokea, wengine, hata watu wa ukoo, hawangeweza tena kusema na yule mvunja-sheria mfu. (Walawi 19:1-4; Kumbukumbu 13:1-5; 17:1-7) Ingawa Waisraeli washikamanifu huko nyuma walikuwa wanadamu wa kikawaida wenye hisia za moyoni kama zetu, wao walijua kwamba Mungu ni mwenye haki na mwenye upendo na kwamba Sheria yake ilitoa himaya kwa usafi wao wa kiadili na wa kiroho. Kwa hiyo wao wangeweza kukubali kwamba kwa msingi mpango wake wa kukatilia nje watenda makosa ulikuwa jambo jema na lenye kufaa.—Ayubu 34:10-12.
-
-
Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye KuamanikaMnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
-
-
a Yohana alitumia khai’ro hapa, ambayo ilikuwa salamu kama “uwe na siku njema” au “jambo.” (Matendo 15:23; Mathayo 28:9) Yeye hakutumia a·spaʹzo·mai (kama katika mstari 13), neno ambalo linamaanisha “kuzungushia kwa kushika katika mikono, hivyo kusalimu, kukaribisha” na huenda likawa liligusia maana ya salamu ya uchangamfu sana, hata pamoja na kumbatio. (Luka 10:4; 11:43; Matendo 20:1, 37; 1 Wathesalonike 5:26) Kwa hiyo mwelekezo ulio kwenye 2 Yohana 11 ungeweza pia kumaanisha kutosema hata “jambo” kwa watu hao.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1986, ukurasa 30.
-