-
Kahaba Mwenye Sifa Mbaya Sana Uharibifu WakeMnara wa Mlinzi—1989 | Aprili 15
-
-
1. Kahaba mkubwa amefanyaje uasherati pamoja na “wafalme wa dunia,” na hiyo imetokeza nini?
YOTE ambayo tumekuwa tukizungumzia ni mazito vya kutosha. Hata hivyo, inatupasa tuangalie kwamba Ufunuo 17:2, NW, unanena juu ya uasherati wa kahaba mkubwa pamoja na “wafalme wa dunia.” Ingawa yeye amepata anguko, angali sana rafiki ya ulimwengu, naye hujaribu kutumia werevu kuwaelekeza watawala walimwengu kama atakavyo ili apate makusudio yake. (Yakobo 4:4) Ukahaba huu wa kiroho, ulio na ngono haramu kati ya Babuloni Mkubwa na watawala wa kisiasa, umetokeza kifo cha mapema cha makumi ya mamilioni ya watu wasio na hatia! Ulikuwa ubaya wa kutosha kwamba kahaba mkubwa alihusika katika pande zote mbili za kupigana katika Vita ya Ulimwengu 1. Lakini kwa uhakika madhambi yake kuhusiana na Vita ya Ulimwengu 2 “yametungamana pamoja moja kwa moja hadi kwenye mbingu”! (Ufunuo 18:5, NW) Kwa nini tunasema hivyo?
2. (a) Franz von Papen alimsaidiaje Adolf Hitler kuwa mtawala wa Ujeremani, na chansela Mjeremani aliyetangulia alielezaje juu ya mheshimiwa huyo wa kipapa? (b) Katika Mapatano kati ya Serikali ya Nazi na Vatikani, ni vifungu gani viwili vya maneno vilivyowekwa kuwa siri? (Ona maelezo ya chini.)
2 Basi, kwa kuchukua kielelezo kimoja, mtawala mkatili Adolf Hitler alikuwaje chansela—na mtawala mtumia mabavu—wa Ujeremani? Ilikuwa ni kupitia mbinu-siasa ya kisiri-siri ya mheshimiwa mmoja wa kipapa ambaye chansela mtangulizi wa Ujeremani, Kurt von Schleicher, alimsimulia kuwa “aina ya haini ambaye Yuda Iskariote akiwa kando yake ni mtakatifu.” Huyu alikuwa Franz von Papen, aliyeiongoza kwa bidii Aksio ya Kikatoliki na viongozi wapinge ukomunisti na kuunganisha Ujeremani chini ya Hitler. Ikiwa ni sehemu ya mapatano ya usaliti, von Papen alifanywa chansela-mdogo. Hitler alipeleka Roma wajumbe wenye kuongozwa na von Papen wakafanye mapatano kati ya Serikali ya Nazi na Vatikani. Papa Pius 11 alieleza wajumbe hao Wajeremani kwamba alifurahishwa sana na jambo la kwamba “sasa Serikali ya Ujeremani ilikuwa na kichwa ambaye ni mwanamume asiyekubali kuuacha msimamo wa kupinga Ukomunisti,” na siku ya Julai 20, 1933, kwenye sherehe yenye madoido mengi katika Vatikani, Kardinali Pacelli (ambaye baada ya muda mfupi angekuwa ndiye Papa Pius wa 12) alitia sahihi mapatano hayo.a
3. (a) Mwanahistoria fulani aliandika nini juu ya Mapatano kati ya Serikali ya Nazi na Vatikani? (b) Wakati wa miadhimisho kule Vatikani, ni heshima gani iliyowekwa juu ya Franz von Papen? (c) Ni fungu gani ambalo Franz von Papen alitimiza katika mpokonyo wa Nazi wa mamlaka ya Austria?
3 Mwanahistoria mmoja anaandika hivi: “Mapatano hayo [pamoja na Vatikani] yalikuwa ushindi mkubwa kwa Hitler. Ulikuwa ndio utegemezo wa kwanza wa kiadili aliokuwa amepokea kutoka ulimwengu wa nje, na isitoshe, kuupata kutokana na chanzo kilichokwezeka zaidi ya vyote.” Wakati wa miadhimisho kule Vatikani, Pacelli alimpa von Papen medali yenye heshima ya juu ya kipapa ya Msalaba Mtukufu wa Daraja la Pius.b Winston Churchill, katika kitabu chake The Gathering Storm, kilichotangazwa kwa chapa katika 1948, anaeleza jinsi von Papen alivyozidi kutumia “sifa yake akiwa Mkatoliki mwema” ili kanisa limuunge mkono kufanya Nazi ipokonye mamlaka ya Austria. Katika 1938, kwa kuheshimu siku ya kuzaliwa kwa Hitler, Kardinali Innitzer aliagiza kwamba makanisa yote ya Kiaustria yapeperushe ile bendera-swastika, yapige kengele zao, na kusali kwa ajili ya mtawala huyo mtumia mabavu wa Kinazi.
4, 5. (a) Kwa nini hatia mbaya sana ya damu inakalia Vatikani? (b) Maaskofu Wakatoliki wa Ujeremani walimuungaje Hitler mkono waziwazi?
4 Kwa hiyo hatia mbaya sana ya damu inakalia Vatikani! Ikiwa sehemu yenye kuongoza ya Babuloni Mkubwa, hiyo ilisaidia sana kumtia Hitler katika mamlaka na kumpa utegemezo “wa kiadili.” Vatikani ilisonga hatua moja zaidi kwa kukubaliana na matendo yake ya unyama kwa unyamavu Wakati wa ule mwongo mrefu wa miaka ya maogofyo ya Kinazi, papa wa Kiroma aliendelea kunyamaza huku mamia ya maelfu ya askari Wakatoliki wakipigana na kufia utukufu wa utawala wa Nazi na huku mamilioni ya maskini wasiojiweza wakimalizwa katika vyumba vyenye gesi vya Hitler.
5 Maaskofu Wakatoliki wa Ujeremani hata walimuunga mkono Hitler waziwazi. Siku ile ile ambapo Japani, mwenzi wa Ujeremani wa wakati wa vita, iliponyemelea na kushambulia Pearl Harbor, The New York Times ilikuwa na ripoti hii: “Mkutano wa Maaskofu Wakatoliki wa Ujeremani waliokusanyika katika Fulda umependekeza ianzishwe ‘sala ya vita’ iliyo maalumu, itakayosomwa mwanzoni na mwishoni mwa ibada zote. Sala hiyo husihi Mungu abariki silaha za Ujeremani kwa ushindi na kutoa himaya kwa maisha na afya ya askari-jeshi wote. Zaidi ya hilo maaskofu hao waliwaagiza makasisi Wakatoliki wawaweke na kuwakumbuka askari-jeshi Wajeremani ‘wa barani, baharini na hewani angalau mara moja kwa mwezi katika mahubiri maalumu ya Jumapili.’”
6. Ulimwengu ungaliweza kuepushwa na maumivu gani yaliyo makali sana na matendo ya unyama kama kusingalikuwa na uasherati wa kiroho kati ya Vatikani na Wanazi?
6 Kama kusingalikuwa na uhusiano wa kimapenzi kati ya Vatikani na Wanazi, huenda ikawa ulimwengu usingalipata yale maumivu makali sana ya kuuawa na vita kwa mamilioni ya askari na raia, kuuawa kwa Wayahudi milioni sita kwa sababu hawakuwa wa asili ya Kiarya, na—jambo lililo la thamani zaidi machoni pa Yehova—kuuawa kwa maelfu ya Mashahidi wake, wapakwa-mafuta na “kondoo wengine” pia, ambao walitendwa matendo ya unyama mkubwa, huku Mashahidi wengi wakifa katika kambi za mateso za Nazi.—Yohana 10:10, 16.
-
-
Kahaba Mwenye Sifa Mbaya Sana Uharibifu WakeMnara wa Mlinzi—1989 | Aprili 15
-
-
KIMYA CHA PAPA
Katika kitabu chake Franz von Papen—His Life and Times, kilichotangazwa kwa chapa katika 1939, H. W. Blood-Ryan anaeleza kirefu mbinu za hila alizotumia mheshimiwa huyo wa kipapa ili kumleta Hitler mamlakani na kufanya ushauriano juu ya mapatano ya Vatikani pamoja na Wanazi. Kuhusu mauaji mabaya sana yaliyopangwa kimakusudi, yaliyohusisha ndani Wayahudi, Mashahidi wa Yehova, na wengine, mtungaji anataarifu hivi: “Mbona Pacelli [Papa Pius wa 12] alikaa kimya? Ni kwa sababu yeye aliona kwamba mpango wa von Papen wa kuwako kwa Milki Takatifu ya Kiroma ya Wajeremani wa Magharibi kungefanya Kanisa Katoliki liwe imara zaidi, huku Vatikani ikiwa imerudia kukalia kiti cha mamlaka ya kidunia . . . Pacelli uyo huyo sasa anatumia mamlaka ya kiroho ya kutawala kimabavu juu ya mamilioni ya nafsi, na bado hata mnong’ono mdogo haukutokezwa kupinga uchokozi na unyanyasi wa Hitler. . . . Ninapoandika mistari hii, siku tatu za machinjo zimepita na hakuna hata sala moja imetoka Vatikani kuombea nafsi za washindani hao, nusu yao hasa wakiwa ni Wakatoliki. Wanaume hawa watatozwa hesabu mbaya sana wakati watakaposimama mbele ya Mungu wao wakiwa wamevuliwa vyeo vyao vyote vya umashuhuri wa kidunia, Naye atawaomba watoe hesabu. Udhuru wao unaweza kuwa nini? Hakuna!”
[Sanduku katika ukurasa wa 15]
-