Je! Wewe Wakumbuka?
Je! wewe umeiona shangwe ya kusoma matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi? Basi, ona kama waweza kujibu maswali yanayofuata:
◻ Ni nini msingi wa ndoa yenye mafanikio?
Ni lazima wenzi wa ndoa waonyeshane upendo, staha, na ushikamanifu, kila mmoja akithamini nguvu za mwenzake za kufanya mema na kujifunza kuachilia na kusamehe udhaifu wa mwenzake.—5/15, ukurasa 15.
◻ Sheria za Mungu walizopewa Israeli ziliwasaidiaje kubaki wakiwa watakatifu?
Sheria za Yehova zilisaidia Waisraeli kubaki wakiwa safi kiroho, kiadili, kiakili, kimwili, na kisherehe, jambo hili la mwisho likiwa ni kuhusiana na ibada yao.—6/1, ukurasa 11.
◻ Usemi “kanuni za afya ya kiakili” wamaanisha nini?
“Kanuni za afya ya kiakili” zamaanisha jitihada ya kimakusudi ambayo sisi hufanya ili tuwe safi katika akili kwa kufanya fikira zetu zidumu juu ya mambo yaliyo ‘ya kweli, ya uadilifu, na ya usafi’ na kwa ‘kuendelea kufikiria mambo haya.’(Wafilipi 4:8)—6/1, ukurasa 6.
◻ kwa nini Yesu alisema kwamba kuwapo kwake kungekuwa “kama vile umeme”? (Luka 17:24)
Hapa Yesu alikuwa akionyesha kwamba uthibitisho wa kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme ungeonwa katika eneo pana, ukiwawezesha wote watakao kuuangalia wawe na habari za uhakika huo.—6/15, ukurasa 8.
◻ kwa nini adabu za Kikristo zahusiana moja kwa moja na upendo wa Kikristo?
Adabu za Kikristo—jinsi sisi hushughulika na wengine, jinsi tunavyojichukua, jinsi tujiendeshavyo, na mwenendo wetu wa kikawaida—na kionyeshi cha jinsi sisi huwajali wengine. Adabu zetu zinaonyesha kina cha upendo wetu kwao. (Yohana 13:35; 1 Wakorintho 10:24; 13:4-7)—6/15, ukurasa 14.
◻ Ndoa ya Yesu na “mkewe” aliye wafuasi waaminifu wapakwa-mafuta 144,000 yatukia lini? (Ufunuo 19:7, 8)
Ndoa hii itatukia kufuatia pigano la Har–Magedoni na kutiwa kwa Shetani katika abiso. Hapo ndipo Yehova atakapokuwa ametetea enzi kuu yake kwa kuwaondoa duniani wale wenye kushindana na utawala wake na kwa kukomesha kabisa uvutano mwovu wa Shetani na roho waovu wake.—7/1, ukurasa 24.
◻ Nira ya uanafunzi yaweza kuletaje burudisho, kama ionyeshwavyo katika maneno ya Yesu kwenye Mathayo 11:29, 30?
Kwa kuwa Yesu si mwenye kutazamia mambo ya kupita kiasi, inaburudisha kufanya kazi pamoja naye tukiwa chini ya nira yake. Yeye huifikiria mipaka ya uwezo wetu na udhaifu wetu mbalimbali. Na inaburudisha kama nini kuambia wengine kwamba wao waweza kuishi milele katika Paradiso!—7/15, ukurasa 20.
◻ Ni nini ‘kuumbwa kupya’ ambako Yesu alinena kwenye Mathayo 19:28, NW?
Hapa Yesu alionyesha kwamba kutakuwa na ‘kuumba kupya’ hali zilizopo duniani ili mambo yawe kama yalivyokuwa katika bustani ya Edeni.—8/1, ukurasa 9.