Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yohana Aona Yesu Aliyetukuzwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 12. Ni nini maana ya ule “upanga mkali, mrefu na wenye makali mawili”?

      12 “Na katika mkono wake wa kulia alikuwa na nyota saba na katika kinywa chake upanga mkali, mrefu na wenye makali mawili ulitokeza, na wajihi wake ulikuwa kama jua wakati linapong’aa katika nguvu zalo. Na mimi nilipoona yeye, mimi nilianguka kama mfu kwenye nyayo zake.” (Ufunuo 1:16, 17a, NW) Baadaye kidogo, Yesu mwenyewe anaeleza maana ya hizo nyota saba. Lakini ebu angalia kinachotokeza katika mdomo wake: “Upanga mkali, mrefu na wenye makali mawili.” Ni sura yenye kufaa kama nini! Kwa maana Yesu ndiye aliyewekwa rasmi atamke hukumu za mwisho za Yehova dhidi ya adui Zake. Matamko yenye kukata maneno kutoka kinywa chake hutokeza kufishwa kwa waovu wote.—Ufunuo 19:13, 15.

      13. (a) Wajihi wa Yesu, mwangavu na wenye kuangaza hutukumbusha sisi nini? (b) Tunapata chapa gani yote kutokana na elezeo la Yohana juu ya Yesu?

      13 Wajihi wa Yesu ulio mwangavu, wenye kuangaza hutukumbusha sisi kwamba uso wa Musa ulitokeza miale yenye kuangaza Yehova alipokuwa amezungumza naye juu ya Mlima Sinai. (Kutoka 34:29, 30) Kumbuka, pia, kwamba wakati Yesu alipogeuka sura mbele ya mitume wake watatu karibu miaka 2,000 iliyopita, “uso wake uliangaza kama jua, na mavazi yake ya nje yakawa maangavu kama nuru.” (Mathayo 17:2, NW) Sasa, katika mwakilisho wa kinjozi wa Yesu katika kipindi cha hii siku ya Bwana, hali kadhalika uso wake unarudisha ubora wenye kung’aa wa mmoja ambaye amekuwa katika kuwapo kwa Yehova. (2 Wakorintho 3:18) Kwa kweli, chapa yote inayopelekwa na njozi ya Yohana ni ile ya mng’ao wa utukufu. Kutoka nywele nyeupe kama theluji, macho yenye kutoa mwali wa moto, na wajihi wenye kung’aa mpaka chini kwenye nyayo zenye mwako, ni njozi yenye ubora unaopita wote ya Mmoja ambaye sasa hukaa “katika nuru isiyoweza kukaribiwa.” (1 Timotheo 6:16) Uhalisi wa tamasha hii ni dhahiri sana! Yohana aliyeshikwa mno na hofu ya staha alitendaje? Mtume huyo anatuambia hivi: “Na mimi nilipoona yeye, mimi nilianguka kama mfu kwenye nyayo zake.”—Ufunuo 1:17, NW.

  • Kufungua Kufuli ya Siri Takatifu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 2. (a) Yesu anajitokeza kwa mtajo gani wa cheo? (b) Ni jambo gani linalomaanishwa wakati Yehova anaposema: “Mimi ndiye wa kwanza na wa mwisho”? (c) Kutaja Yesu kuwa “wa Kwanza na wa Mwisho” kunavuta fikira kwenye jambo gani?

      2 Hata hivyo, hofu yetu haipasi kuwa woga wa kufisha. Yesu alimtuliza Yohana, kama vile mtume huyo anavyosimulia yanayofuata: “Na yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu mimi na akasema: ‘Usiwe mwenye hofu. Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho, na yeye aliye hai.’” (Ufunuo 1:17b, 18a, NW) Katika Isaya 44:6, NW, kwa kufaa Yehova anakieleza cheo chake kuwa ndiye Mungu mweza yote mmoja tu na wa pekee, akisema: “Mimi ndiye wa kwanza na wa mwisho, na mbali na mimi hakuna Mungu.”a Yesu anapojitokeza mwenyewe kwa mtajo wa cheo “wa Kwanza na wa Mwisho,” yeye hadai kuwa yu sawa na Yehova, yule Muumba Mtukufu. Yeye anatumia mtajo wa cheo aliopewa kwa kufaa na Mungu. Katika Isaya, Yehova alikuwa akitoa taarifa kuhusu cheo Chake kisicho na kifani akiwa ndiye Mungu wa kweli. Yeye ni Mungu milele, na mbali na yeye hakuna Mungu kweli kweli. (1 Timotheo 1:17) Katika Ufunuo, Yesu anazungumza juu ya mtajo wake wa cheo ambao amepewa, akivuta fikira kwenye ufufuo wake usio na kifani.

      3. (a) Ni katika njia gani Yesu alikuwa “wa Kwanza na wa Mwisho”? (b) Ni jambo gani linalomaanishwa na Yesu kuwa na “funguo za kifo na za Hadesi”?

      3 Yesu alikuwa kweli kweli ndiye binadamu “wa Kwanza” kufufuliwa kwenye uhai wa roho usioweza kufa. (Wakolosai 1:18) Na zaidi, yeye ndiye “wa Mwisho” kufufuliwa hivyo na Yehova binafsi. Hivyo, yeye anakuwa ‘aliye hai, ambaye anaishi milele na milele.’ Yeye anajifurahisha kutokufa. Katika jambo hili, yeye ni kama Baba yake asiyeweza kufa, ambaye anaitwa “Mungu aliye hai.” (Ufunuo 7:2; Zaburi 42:2) Kwa wengine wote wa ubinadamu, Yesu mwenyewe ndiye ‘ufufuo na uhai.’ (Yohana 11:25, NW) Kupatana na hili, yeye anasema kwa Yohana hivi: “Mimi nilipata kuwa mfu, lakini, tazama! mimi ninaishi milele na milele, na mimi nina funguo za kifo na za Hadesi.” (Ufunuo 1:18b, NW) Yehova amempa yeye mamlaka ya kufufua wafu. Hiyo ndiyo sababu Yesu anaweza kusema kwamba yeye ana funguo za kufungua kufuli za malango kwa ajili ya wale ambao wamefungwa na kifo na Hadesi (jumla ya makaburi).—Linga Mathayo 16:18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki