-
Uongozi Wenye Kutenda wa Kristo LeoMnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
-
-
Waangalizi Katika Mkono wa Kuume wa Kristo
8, 9. (a) Ni njozi gani aliyopokea mtume Yohana? (b) Ni nini kilichofananishwa na vinara vya taa saba na nyota saba?
8 Mtume Yohana, mshiriki wa baraza lenye kuongoza la kundi la Kikristo la kwanza, alipokea njozi ambayo katika hiyo ‘aliona vinara vya taa saba vya dhahabu; na katikati ya vile vinara aliona mtu mfano wa Mwanadamu . . . Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume.’ Yesu Kristo alimweleza Yohana hivi: “Siri [takatifu, NW] ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya dhahabu. Zile nyota saba ni malaika wa yale [makundi, NW] saba.”—Ufunuo 1:12-20.
9 Kikitoa maelezo juu ya fungu hili la maneno, kitabu “Then Is Finished the Mystery of God” kinasema: “Je! ‘malaika’ hawa ni wale wasioonekana? Hapana. Mtume Yohana alipokea ufunuo wote kutoka kwa Yesu Kristo kwa njia ya malaika wa kimbingu, na lingekuwa jambo lisilopatana na akili kwake kuwa akiandikia tena malaika katika mbingu, katika makao yasiyoonekana. Wao hawahitaji ujumbe mbalimbali ulioandikiwa yale makundi saba katika Esia. Maana ya msingi ya jina la cheo ‘malaika’ ni ‘mjumbe; mchukuaji wa ujumbe.’ . . . Kwa kuwa hizi nyota saba za mfano zinaonekana zikiwa juu ya mkono wa kuume wa Yesu, ziko katika uangalizi na amri yake na chini ya mwelekezo wake, ‘mkono wa kuume’ wake wa uweza unaotumiwa ukiwa unaweza kuzielekeza na kuzilinda. . . . Kama vile vile ‘vinara vya taa saba’ katika ‘siku ya Bwana’ ya kinjozi vilivyofananishwa na makundi yote ya Kikristo ya kweli katika hii ‘siku ya Bwana’ halisi, ya sasa tangu 1914 W.K., ndivyo zile ‘nyota saba’ zinavyofananisha waangalizi wote wa makundi hayo ya leo waliozaliwa kwa roho, wapakwa-mafuta wenye mfano wa malaika.”b —Kurasa 102-4.
10. Ni “mali” gani zilizoongezeka ambazo zimewekwa kwenye uangalizi wa mtumwa?
10 Waangalizi hao wapakwa-mafuta walio katika mkono wa kuume wa Kristo wote ni sehemu ya jamii ya yule “mtumwa” ambaye Yeye ameweka “juu ya mali zake zote.” Kwa sababu mtumwa wa Bwana mwenyewe amevikwa madaraka yaliyopanuliwa tangu 1914, “mali zake zote” lazima zihusu vitu vingi zaidi kwa mtumwa kuliko katika wakati uliopita. Jambo moja ni kwamba, wakiwa “mabalozi badala ya Kristo,” sasa mabaki ni mabalozi wa Mfalme anayetawala akitawala juu ya Ufalme uliosimamishwa. (2 Wakorintho 5:20, NW) Wamekabidhiwa mambo yote ya kiroho ambayo ni mali ya Bwana duniani. Ni lazima wao watumike katika utimizo wa unabii mbalimbali unaohusika tangu kusimamishwa kwa Ufalme. Huo unatia ndani kuhubiri “habari njema hizi za ufalme . . . katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda.” (Mathayo 24:14, NW) Zaidi ya wakati mwingine wo wote, ni lazima waendelee kufanya “wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,” hivyo kukusanya ndani ule “mkutano mkubwa” usio na hesabu. (Mathayo 28:19, 20, NW; Ufunuo 7:9) Ndiyo, hivi “vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote” ni sehemu ya “mali” za Kristo zilizoongezeka duniani.—Hagai 2:7.
11. (a) “Mali” hizo zilizoongezeka zilifanya jambo gani liwe la lazima kabisa? (b) Ni nani anayeelekeza kazi, na jinsi gani?
11 Yote haya yanamaanisha kazi zaidi kwa jamii ya “mtumwa,” eneo kubwa zaidi la utendaji, likienea kihalisi kufika “dunia yote inayokaliwa na watu.” Inahitaji pia makao makuu makubwa zaidi na vifaa vya tawi kwa ajili ya kusimamia kazi na kwa kazi ya uchapishaji na uenezaji wa vitabu vya kutumia katika kuhubiri na funzo la kibinafsi. Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, kazi hii inaendeshwa chini ya uongozi wenye kutenda wa Yesu Kristo, ambaye kwa njia ya mfano yumo “katikati ya vile vinara [vya taa, NW],” au makundi. Yeye anayaelekeza kwa njia ya waangalizi wapakwa-mafuta, ambao yeye kwa kwa njia ya mfano anawashika “katika mkono wake wa kuume.” (Ufunuo 1:13, 16) Kama ilivyokuwa katika nyakati za Ukristo wa kwanza, kikundi cha hawa waangalizi wapakwa-mafuta wanajumlika kuwa Baraza Linaloongoza lionekanalo la kundi la Kristo duniani. “Mkono wa kuume” wake wa uwezo unaotumiwa unaelekeza hawa wanaume waaminifu wanaposimamia kazi ya Ufalme.
-
-
Uongozi Wenye Kutenda wa Kristo LeoMnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
-
-
b Toleo la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 1972, lilifafanua jambo hili hata zaidi, likisema: “Bila shaka, si mzee mmoja, mwangalizi au mchungaji mmoja, bali ‘baraza ya wazee,’ yote ndiyo Bwana Yesu Kristo aliyetukuzwa, aliiita ‘malaika’ aliyefananishwa na nyota ya mbinguni. . . . ‘Baraza la wazee’ kule Efeso ilipaswa itende kama nyota katika kutoa nuru ya kimbinguni, ya kiroho juu ya kundi ambalo juu yake roho takatifu ilikuwa imewafanya kuwa wachungaji.”
-